Tanzania (SCT) Yatwaa Kombe la Dunia la Vijana wa Mitaani- 2014.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Dk. Fenella Mukangara (kushoto) na 
Waziri wa Ardhi, Nyumbana Maendeleo ya
 Makazi,Profesa Anna Tibaijuka wa pili (kulia)
wakiwa pamoja na timu hiyo
Mapema ndani  ya wiki la kwanza la mwezi  wa nne 2014 Tanzania iliandika histori baada ya timu ya Watoto wa mitaani Tanzania  (SCT) kulitwaa kombe la Dunia  la vijana wa mitaani kule Rio de Jeneiro Brazil.

Timu hii ililitwaa kombe hili kwa baada ya kuichapa timu ya watoto wa mitaani ya Burundi mabao matatu kwa nunge (3-0).

Timu hii ya Burundi iliingia fainali katika michuano iliyohusisha  vijana 230 toka nchi 19 katika lengo la kuwaleta watoto katika nchi hizi karibu.

Ushindi huu haukupatikana kirahisi kwani ulipatikana baada ya timu hii kuzishinda timu nyingine  kadhaa zinazosifika katika kandanda duniani kama vile Argentina  marekani na nyingine .  

Hii ni ishara tosha kwamba vijana hawa wana vipaji na vikiendelezwa wanaweza kuifanya Tanzania kutimiza ndoto yake ya kuchukua kombe la kandanda la dunia.

 Ijumaa ya tarehe 11,Aprili 2014 Friday, April 11, 2014Timu ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania iliyotwaa Kombe la Dunia mwaka huu ilitembelea Bunge maalumu la katiba na kuiomba Serikali kuwasaidia

Juhudi za vijana hawa zilianza kuonekana mapema toka mwaka 2010 pale walipoingia fainali na India katika michuano kama hii hii na kushindwa.
Licha ya matatizo mbalimbali yanayowakabili Watoto hawa wa Mitaani wamethibitisha kwa vitendo kuwa hakuna lisilowezekana kama kutakuwa na nia.
 Kinachorudisha juhudi zao nyuma ni kukosa taasisi au watu wa kuwashika mkono kwa maana ya kuendeleza vipaji vyao.
Mkurugenzi wa Timu ya Watoto wa
 Mitaani (TSCSA), Mutani  Yangwe akisalimiana
 na Makamu wa pili  wa Rais wa Zanzibar,
Balozi Seif Ali Iddi mjini Dodomamara baada ya  timu  hiyo na viongozi wao kutembelea Bunge Maalum la Katiba
Kwa hili, tunaipongeza sana Taasisi ya Tanzania Street Children Sports Academy (TSCSA) ya jijini Mwanza Rais wa kituo hiki Altaf Hirani, na Mkurugenz wake Yangwe Mtani kwa kuwajumuisha pamoja watoto hawa na kuwashughulisha katika shughuli mbalimbali zikiwamo za michezo.
“Kupitia michezo kama hii watoto hawa wanaweza kuonesha vipaji vyao katika kumudu soka na huu ni mfano halisi kuwa kumbe hawa watoto wa mitaani wanaweza kufika mbali na kufanya mambo makubwa katika michezo iwapo watasaidiwa.” Rais wa kituo hiki Altaf Hirani alisema.

 Mfungaji bora wa  timu hii ya Watoto wa Mitaani kutoka  Mwanza Tanzania, (TSC) ambayo iliibuka mshindi katika mashindano haya ya Kombe la Dunia la  Watoto yaliyofanyika Brazil, mwaka huu  Frank William ameishauri , Serikali na jamii kuwasaidia ili kujiandaa na mashindano kama haya.

Kauli hiyo ilitolewa leo mjini Dodoma na  William  ambaye pia alikuwa Capteni katika timu hii wakati walipolitembelea Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma ambapo walipata nafasi ya kuzungumza na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara pamoja na Naibu wake  Juma Nkamia na viongozi wengine mbalimbali akiwemo waziri mkuu Pinda ambaye aliandaa chakula cha pamoja na watoto hawa.

Alisema  siri ya ushindi wetu ni ushirikiano na kujituma. Hivyo  aliomba jamii kuwasaidia watoto wengi wa mitaani ambao hawana uwezo wa kupata  elimu lakini wana vipaji mbalimbali ili waweze kuvikuza.

Kwa upande wake kipa bora wa timu hiyo, Emmanue  Amos, alishauri Serikal iweze kuwasaidia ili waweze kushiriki katika mashindano ya mwaka 2018 ya  kombe  hilo.

Mchezaji mwingine wa timu hiyo, Denis David aishauri jamii isiwadharau kwa kuwa ni watoto wa mitaani kwani wanavipaji. Aliitaka jamii kuwekeza katika  soka la vijana  kwa  sababu baada ya miaka 20 ijayo mchezaji bora atapatikana kwa njia hiyo.

Naye Kocha wa timu hiyo, Suileiman Jabir aliwataka wadau  mbalimbali  kuwasaidia na  kuwaendeleza watoto hawa ambao wengi wameonesha wana  vipaji vya sanaa na utamaduni.

Akizungumzia kuhusu mafanikio ya ushindi kama huu hapo baadae  alishauri kuweka mpango wa kutafuta vijana wenye vipaji ambapo wataviendeleza na kuvikuza kwa kufanya maandalizi ya kiutalaamu na kiufundi. Jabir aliongeza kuwa waliwaandaa  watoto hawa kisaikolojia ili waweze kushinda katika mashindano hayo ya kimataifa.

Alishauri saula la watoto kupewa kipaumbele na kuweka sheria itakayowadhibiti wakina baba wanao telekeza watoto na kuiasa jamii kuwasaidia watoto pale wazazi au walezi wanapofariki dunia. 

Rais wa timu hii ya Watoto wa mitaani  Altaf Hirani aliiomba Serikali kuwasaidia kupata kiwanja  cha michezo  kwa ajili ya watoto hawa jijini Mwanza au kwenye  maeneo mengine ya nchi. 

 Naye Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Michezo na Utamaduni Juma Nkamia akizungumzia kuhusu timu hiyo alisema ameliagiza Shirikisho la Mchezo wa Soka  Tanzania (TFF) kuwa na mpango endelevu wa kuwasaidia watoto.
Wadau mbalimbali nchini kuanzia Serikali, wanapaswa kuona umuhimu wa kuwasaidia watoto katika maeneo mbalimbali nchini kuendeleza vipaji walivyojaliwa na Mwenyezi Mungu.
Ushindi wa Watoto wa Mitaani wa kutwaa Kombe la Dunia ni kielelezo kwamba Tanzania imejaliwa vipaji vingi katika michezo, lakini tatizo kubwa limekuwa ni jinsi ya kuviibua vipaji hivyo na kuviendeleza.
Kinachotakiwa sasa ni Serikali kwa kushirikiana na taasisi nyingine zisizo za kiserikali kama TSCSA kubeba jukumu hili na kuhakikisha ndoto za vijana wetu zinatimizwa.
Hongera sana Watoto wa Mitaani. Mmeipeperusha vyema Bendera ya Tanzania.

Vyanzo: TV, Magazeti na mitandao ya kijamii.




0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza - Blogger Theme by SoraTemplates