Mazishi ya Gwiji la Muziki Maalim Muhidin Gurumo Yahudhuriwa na Maelfu ya Watu.

Marehemu Muhidin Maalimu Gurumo
Mazishi ya gwiji la muziki wa dansi  nchini Muhidin Maalimu Gurumo, aliyefariki Jumapili Aprili 13, 2014  na kuzikwa siku ya  Jumatano tarehe 15 Aprili 2014  kijijini kwake  Masaki Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani yahudhuriwa na maelfu ya watu.

Mauti ya nguli huyu wa muziki wa dansi nchini yalimfika akiwa katika matibabu ya ugonjwa wa moyo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alikokuwa amelazwa.

Ugonjwa wa moyo umemsumbua kwa kipindi kirefu.Na huenda ndio uliopelekea hata  akatangaza kustaafu shughuli za muziki.

Alipata elimu ya msingi shule ya msingi Sungwi, Masaki Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani huko.

Alisoma madrasa, chuo cha kufundisha elimu ya Dini ya Kiislamu enzi za udogo wake.
Baada ya baba yake kufariki aliacha shule na  alichukuliwa na mjomba wake  Selemani Sultani Mikole, ambaye wakati huo alikuwa akiishi maeneo ya Ilala Jijini Dar es Salaam.

Gurumo alipoacha shule  alianza kupiga muziki na bendi za mitaani alianza na bendi iliyojulikana kama Scock Jazz iliyokuwako mitaa ya Moshi na Kigoma.

 Baada ya mwaka mmoja katika bendi hii alijiunga na  bendi ya kilimanjaro Chacha ambayo ilikuwa na vyombo vya muziki vya kisasa. Katika bendi hii alitunga vibao vya;Twende Tukalime,Mapenzi Hayana Dawa,Ushirikina ni Sumu na Maendeleo.

Mwaka 1963 alijiunga na Rufiji Jaz Band na hapa alitunga kibao kilichompa umarufu katika muziki wa dansi kijulikanacho kwa jina la Uwezo wa binadamu kufikiri.

Mwaka huo huo alijiunga na Kilwa Jazz Band hapa alitoa vibao vilivyovuma enzi hiyo vya Wewe Mpenzi Naomba Unishauri Kabla Hatujagombana na Siwezi Kukununulia Gari Wakati Hata Baisikeli Sina.

Mwaka 1964 alikuwa miongoni mwa walioanzisha   bendi ya Nuta Jazz wakati huo akiwa na kina Ahmed Omary, Mohamed  Omary,Epimakus Mkundika na Rashid Abdallah (Wengine wa hai na wengine  ni marehemu sasa)

Akiwa Nuta Jazz Bandi alitunga vibao vingi ila hivi viliuma navyo ni Magdalena,Maneno ya Mwalimu Maneno ya Wazee yote Sawa na Rehema Umefeli Shule kwa Sababu Gani.
Baadae Nuta Jazz Bandi iliitwa OTTU Jazz  Band kutokana na mabadiliko yaliyotokea  kipindi hicho katika vyama vya wafanyakazi nchini.

Akiwa OTTU  alitoa vibao  vingi  ila vilivyovuma sana ni Tenda wema na usia kwa watoto.
Kama Simba walivyo watani wa Yanga katika soka Msondo Ngoma  (Baba ya Muziki) watani wao kimziki  ni DDC Ochestra Mlimani Park

Raisi akimfariji mjane wamarehemu Muhidin Maalim 
Gurumo
Mapema JIONI  baada ya maziko Raisi  Mhe. Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete alifika nyumbani kwa marehemu kutoa rambirambi na mkono wa pole.

Pichani Raisi anaonekana akimfariji mjane wa marehemu Muhidin Maalim Gurumo (mwenye shuka nyeupe) na wanafamilia pale alipokwenda kuhani msimba huo Ubungo Makuburi jioni ya April 15, 2014, siku ambayo marehemu alizikwa kijijini kwao Masaki, Kisarawe, Mkoa wa Pwani.

Msafara wa kwenda malaloni uliongozwa na Makamu wa Rais  Dk. Mohamed Gharib Bilal.Aidha msafara huu ulianzia nyumbani kwake Mabibo, Makaburi Jijini Dares salaam (kwa jina jingine maarufu la mtaa huu Tabata External )baada ya  kutolewa kwa heshima za mwisho na kupokelewa kwa salamu kutoka makundi mbalimbali.

Magari zaidi ya 20 yalianza msafara huu saa 05:15  kwenda Masaki na yalifika kijijini kwake  saa 7:10 adhuhuri.

Mwili wa marehemu ukipelekwa
katika nyumba yake ya milele
Kabla ya Mwili wa Gurumo kupelekwa malaloni, ulipelekwa kwanza  msikitini kuswaliwa na
baada ya kuswaliwa mmwili ulipelekwa makaburini  ndani ya jeneza tayari kwa maziko.

Baada ya marehemu kuswaliwa  kunako  saa 07:40 mwili ulipelekwa makaburini  hapo  karibu na nyumbani kwao   hapo hapo Masaki mkabala na ilipo nyumba alikozaliwa.

Mwili ukingizwa kaburini
Makaburini Kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma Saidi Mabela na ndugu wa marehemu waliingia kaburini kuulaza mwili wa Marehemu Gurumo kwenye nyumba yake ya milele.

Kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma Mabela alisema pamoja na Gurumo kujiuzulu muziki walikuwa wote katika bendi ya OTTU  hadi pale mauti yalipomfika.

Aliongeza kuwa marehemu akiwa Meneja wa bendi kwa hiyo mauti yamemkuta Gurumo akiwa pamoja naye  katika  bendi.

Mmoja wa wanamziki hapa nchini amemtaja  Marehemu Maalim Muhidini Gurumo kuwa ni Mwalimu wa wanamuziki wengi hapa nchini na kwamba  amewainua wanamziki wengi hadi kuwa maarufu katika fani hiyo.

Muhidini Maulidi Gurumo amekuwa katika bendi kadhaa kama  ilivyofafanuliwa  hapo juu enzi za uhai wake kabla ya kuanzinsha bendi yao ya Msondo Ngoma.

 Aliwahi kupigia Bendi ya OSS (Ochestra Safari Sound) na DDC Mlimani  Park maarufu kwa jina la mtindo wao wa Ndekule.

Mwana muziki King Kiki akiwa na wadau wa muziki.
Mwana muziki King Kiki alimweleza Gurumo kuwa ni mwanamuziki  aliye kuwa na kipaji cha kipekee katika utunzi.Alisema alikuwa na uwezo wa kutunga wimbo hapo hapo na kuimba akaongezea  kuwa  ni  yeye aliyebuni mitindo ya Ndekule na Msondo.

Mwanamuziki  Ali Choki kiongozi wa bendi ya Extra Bongo ni miongoni mwa wanamziki waliopata ujuzi na kufanya kazi pamoja na Marehemu Gurumo.

Choki anamtaja marehemu kama Mwalimu Mkuu wa Muziki nchini ambaye sasa ametoweka katika ulimwemuzikingu kwa kusema; "Gurumo ni mwanamuziki aliyekaa kwenye 'game' kwa siku nyingi, ninashauri wanamuzuki wa kizazi hiki kufuata nyendo, heshima na mambo mazuri aliyoyaishi. mkongwe huyu katika tasinia ya muzuki"

Aidha mastaa mbalimbali wa tasinia mbalimbali akiwemo  JB mmoja wa waingizaji  maarufu nchini alisema pengo aliloacha Gurumo litatuchukua kipindi kirefu kuliziba.

Mwanamziki huyu wengi wanadai  alitabiri kifo chake kwa yale aliyofanya  kabla ya kifo chake,  

Akiwa kalazwa aliondoka wodini mara kadhaa akidai  kutolewa hasipitalini arudishwe nyumbani kwake. Jingine ni pale alipoagiza agiza wanae siku chache kabla ya kulazwa, waende huko Masaki kusafisha makaburi  ya ukoo, Jingine ni lile la kutangaza kuacha kupiga muziki.
Diamond Platinum Akimkabidhi Maalimu Gurumo
Enzi za Uhai wake Ufunguo wa Gari

Kitenndo chake  hiki cha kutangaza kuacha  muziki kilipelekea Diamond Platinum kumpa Gari hasa pale alipolalamika katika mahojiano yake na TBC kuwa anaacha muziki huku akiwa hana kitu cha kujivunia kutokana na tasinia hii ya muziki.

Mwanamziki  Gurumo (Kamanda wa muziki ) kama mashabiki wa muziki walivyokuwa wakimwita  ilizaliwa mwaka 1940 katika Kijiji cha Masaki Wilaya ya Kisarawe Mkoa wa Pwani na amefariki akiwa na miaka 74..

Mjane wa marehemu Guromo
Marehemu Maalim Muhidin Gurumo alioa na  ana watoto, wajukuu na vitukuu. Pia alikuwa ni mwanachama wa  Klabu ya Simba tangu 1964.

"Sisi sote tumetoka kwa Allah (SW) na marejeo yetu sote ni kwake" (INNA LILLAIHI WA INAILLAIHI RAJIUUN)

Mungu ilaze roho ya marehemu Gurumo mahali pema peponi

Ona video ya mazishi ya Marehemu Muhidin Maalimu Gurumo ijijini Kwao MASAKI Kisarawe wilaya ya Pwani.(Video imeandaliwa na Global TV)




Source:.bongocelebrity  na vyanzo mbalimbali vya habari

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza - Blogger Theme by SoraTemplates