Watu Wanne Wauawa na Wananchi Waliokuwa na Hasira Kali.

Mmoja wa walio uliwa akipata kipigo
Watu wanne wauawa na wananchi waliokuwa na  hasira kali kwa silaha za jadi kisha kukatwa katwa mapanga  kwa tuhua  za kuiba ng'ombe.

Haya yalitokea katika kijiji cha Igwambiti, Kitongoji cha Buhongwa, Kata ya Nyamagana, hapa jijini Mwanza jana asubuhi tarehe 18,March 2014.

Mtendaji wa kata ya Buhongwa Benedict Kabadi alisema  alipokea taarifa za kutokea mauwaji haya jana asubuhi na alipofika eneo la mauaji hayo alikuta miili ya watu watatu waliouliwa.

Alidai wananchi walimkamata Joseph Mwita na kumtaka awaoneshe watu anaoshirikiana nao katika wizi.Inadaiwa aliwapeleka hadi kijiji cha Igwambiti katika kata hii na kuwaonesha.
Mtendaji Kabadi anasema watuhumiwa hawa waliuwawa na kundi la watu.Alipofika eneo la tukio walikuwa wameisha ondoka na kuacha miili hiyo hapo.

Baadae ilifahamika kuwa waliouliwa ni Ezekieli Lucas (27),Kusekwa Lucas (25),Masumbuko Kisinza (30) wote wakiwa ni wa kazi wa kijiji hiki cha Igwambiti katika kata hii ya Buhongwa. Wilaya ya Nyamagana na Mfanya biashara ya nyama wa Buhongwa,Mafisi Mwita (30).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Valentino Mlowola anasema watu watatu wanashikiliwa na jeshi hilo kwa kukutwa na marungu yenye damu.

Akifafanua zaidi alisema tukio hilo lilitokea jana hiyo majira ya saa11.30 alfajiri katika kijiji hicho cha Igwambiti Kata ya Buhongwa.

Chanzo cha mauaji haya inadaiwa ni wizi wa ngo'mbe uliotokea katika kitongoji cha Nyang'omango katika kijiji cha Mtende Tarafa ya Usagara,Wilaya ya Misungwi.

Akikemea hatua hii ya wananchi kujichukulia madaraka mikononi Kamanda Mlowola  akihojiwa na kituo cha luninga cha Star, hapa jijini Mwanza alisema uchunguzi juu ya mauaji haya unaendelea ili kubaini wote waliohusika katika mauaji haya.

Hatusemi wezi wa ng'ombe wauliwe wakikamatwa lakini hatua za kukomesha wizi wa ngo'mbe  hususani hapa jijini Mwanza umekithiri hivyo tunaliomba jeshi letu la Polisi lione hili kama tatizo katika mkoa wetu na liongeze juhudi za makusudi kukomesha wizi huu.

Chanzo: clouds fm

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza - Blogger Theme by SoraTemplates