Mkazi Mmoja Maeneo ya Butimba Tambuka Reli Ang'oa Dirisha la Nyumba ya Jirani.

Mbwa aliyekutwa na mpiga picha akijitafutia
 chakula jalalani  (Picha na Mwl.Msangi E.H.)
Mkazi  mmoja maeneo ya Butimba Tambuka Reli ang'oa dirisha la nyumba ya jirani akimkimbia mbwa.

Ilikuwa ni siku ya Alhamisi, tarehe 20 Marrch 2014  majira ya  Mchana wiki iliyopita, kundi kubwa la watoto  wa ButimbaTambuka -Reli mtaa wa Kanyerere.Wilaya ya Nyamagana Jijini  Mwanza walikuwa wakimshambulia mbwa.

Kwa mafimbo,magongo na mawe  watoto  hawa walimshambulia mbwa huyu kwa lengo la kumuua kwa kumdhania ana kichaa cha mbwa kwa hali dhoofu aliyokuwa nayo.

Tendo hili lilitokea katika moja ya barabara  za kitongoji hiki cha Butimba Tambuka- Reli.

Akimsimulia mwandishi wa kisa hiki, Mratibu wa Elimu kata  ya Butimba Ndugu Rogasian N, Mrema alisema habari hii ilipatikana  ofisini  kwake  wakati wakisimuliwa  kisa kingine kama hiki cha kijana kukimbizwa na mbwa  na kugonga mti kwa kichwa  maeneo  hayo hayo ya Tambuka-Reli.

Katika kisa hiki inasemekana kijana alipogonga mti kwa kichwa mbwa aliyekuwa anamkimbiza alipoona hivyo akaogopa kuwa kama atagongwa naye hivyo itakuwa hatari kwake hivyo akajiondokea.

Kwa kisa hiki cha kung'oa dirisha . Mwenyekiti wa  kitongoji hiki cha Butimba Tambuka Reli kilikotokea Ndugu Leonard Malisa ambaye ni Ndugu wa Bwana Mshiu Dominic  aliyekimbizwa, alisema Bwana Dominic Mshiu  akiwa njiani kuelekea nyumbani aliona kundi la watoto wakimshambulia mbwa kwa kusudio la kumuuwa.

Bwana Mshiu hakujishughulisha nao akajipitia kwenda alikokuwa akielekea . Mara alishitukia  mbwa anamkimbilia.Wengi wanahisi mbwa huyu alikuwa anatafuta msaada kwake.

Naye kuona mbwa anakuja mbio kwake akaogopa na kuongeza kasi kumkimbia. Mbwa  naye akaongeza kasi ili asiachwe kwa wale watoto walio kuwa wakimpiga.

Bwana huyu alipoona mbwa anamkaribia.akaongeza mbio huku akipiga kelele za kuomba msaada.

Pamoja na mbio hizi  bado mbwa alikuwa karibu sana naye .

Kwa kuona hawezi kumwacha kwa mbio  mbwa huyu, alipokaribia nyumba ya mama mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Mama Kanyerere. bila hodi  huku akipiga  yowe aliingia ndani ya nyumba hii.

Alipoingia na mbwa  naye akaingia. Kuona hivyo akaingia chumbani.Mbwa hakuchelewa haraka haraka  kabla hajarudishia mlango wa chumba  mbwa naye  huyo chumbani.

Kuona hivyo Bwana Mshiu Dominic  akapiga ngumi dirisha la chumba hicho na kutoka nalo.Akiwa nje bado akaona kama  haitoshi hiyo kwa usalama zaidi akapanda  juu ya mti wa mwembe uliokuwa hapo karibu.

Mama mwenye nyumba kwa sasa inasemekana anadai dirisha lake likarsbatiwe ama kama  sivyo anatishia kumfungulia bwana  Dominic  mashitaka.

Habari ambazo hazijathibitishwa zadai ni kwamba mbwa huyu ameuliwa kwa kwa hofu kwamba huenda anaweza kuleta madhara  kwa wakazi wa eneo hili.

Kwa upande mwingine wanadai mbwa huyu hakuwa na kichaa bali alikuwa anatafuta nusura toka kwa bwana Mshiu, kwani kama alikuwa akitaka kumuuma asingeshindwa kwa vile  alikuwa anamkaribia mno kiasi ambacho  asingeshindwa kumuuma kama hilo ndiyo lilikuwa kusudio lake.

Tukio hili lapaswa liwe fundisho kwa jamii.Ufugaji holela wa mbwa unatakiwa kukomeshwa.TuwafungIe mbwa vibandanI nyakati za mchana. Mbwa wasiachwa  na wanaozagaa ovyo wauliwe.Isitoshe idara ya mifugo inapaswa kufanya juhudoi kuchanja mbwa wote na mbwa anayeonekana kuzagaa auliwe.

Kinga ni bora kuliko tiba.

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza - Blogger Theme by SoraTemplates