Rais wa Malawi adai kuwa ni mahakama pekee ndiyo iwezayo kuamua mgogoro wa matokeo ya kura nchini humo.

Aliyeko kutokea kushoto ni  Chief Justice Richard Banda, mkewe akifuatia  Joyce Banda Raisi wa  Malawi. Aliyeketi mbele ni Anjimile mpigisha kura. Wakiwa msitarini kupiga kura  Katika jimbo la Zomba, Malawi, Jumanne,ya Mei 20, 2014 Bi Joyce Banda Alipambana na Wagombea12 Katika Uchaguzi huu.

Rais wa Malawi adai kuwa ni  mahakama pekee ndiyo  iwezayo kuamua mgogoro wa matokeo ya kura nchini humo.


Lilomgwe Malawi  - Rais wa Malawi Joyce Banda alisema jana Alhamisi, 29,Mei 2014 kwamba yuko tetayari kuachia ngazi kama Mahakama Kuu itaridhia kuwa uchaguzi wa wiki iliyopita ambako mpinzani wake anadaiwa kuwa na kura zaidi utarudiwa. 

Mpinzani wake huyu anaonekana ndiye  mshindi.Banda hakubaliani na matokeo kwa kudai kuwa kura zilihesabiwa kwa udanganyifu.

Mahakama Kuu ilitarajiwa kutokana hukumu leo siku ya Ijumaa Hukumu ambayo ingeiwezesha Tume ya Uchaguzi ya Malawi (MEC)  kutangaza matokeo ya Mei 20  ambayo mpinzani wa Banda ndiye aliye na uwezekano wa kuwa mshindi, au kurudia zoezi la uhesabuji upya,  mchakato ambao unaweza kuchukua muda wa miezi miwili.

Nchi hii ya kusini mwa Afrika inayokabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi inasubiri uamuzi huu wa kimahakama wa ama Tume itangaze matokeo yaliyopatikana au  kurudia uhesabuji wa kura upya. 

Uanuzi ambao unaweza kuleta ghasia katika uchaguzi huu wa  mfumo wa vyama vingi toka  ule wa chama kimoja uliokuwepo tokea miongo miwili iliyopita.

"Nimewaambia MEC  na wadau kwamba mimi nitaukubali uamuzi wa mahakama, " Banda aliiambia Reuters alipofanya mahojiano nao katika mji mkuu wa Malawi Lilongwe.

"Mimi nilitoa uhuru ili uchaguzi uendeshwe kwa misingi ya haki, uhuru na usawa.Yote haya ni   katika  kutetea haki ya wananchi wa Malawi katika wakati huu muhimu ili  kuhakikisha kuwa kiongozi anayechaguliwa anachaguliwa kwa njia ya haki na kuaminika, " aliongeza.

Uchaguzi ulikumbwa na matatizo mengi. Vifaa vya kupigia kura vilifikishwa vituoni kwa kushelewa  na karatasi nyingine za kupigia kura zilipelekwa kwingine . 

Tume ya Uchaguzi (MEC) ililazimika  kuongeza muda wa  kupiga kura katika baadhi ya maeneo ya mijini ndani ya siku ya pili na uhesabuji wa  awali ulifanyika nje ya muda tena kukiwa na ukosefu wa umeme katika baaddhi ya vituo vya kupigia kura,

Katika siku  nne za awali za uhesabuji  (MEC)Tume ya Uchaguzi ilionesha kuwa Chama cha upinzani cha Democratic Progressive Party (DPP ) kinachoongozwa na Peter Mutharika , ndugu wa marehemu Rais Bingu wa Mutharika kilikuwa  kukiongoza kwa asilimia 42 ya kura zilizopigwa.

Banda, Aliyekuwa Raisi wa kwanza  mwanamke Kusini mwa Afrika, alikuwa akifuatia kwa asilimia 23. 

Uhesabuji wa kura umemalizika lakini Tume bado haijatangaza matokeo.


Taarifa za vyombo vya habari vya nchini Malawi  zinadai kwamba Mutharika bila shaka atachukua ushinda kama hakutakuwepo na urudiaji wa kupiga kura. .

Baada ya kushauriana na vyama viwili vya  upinzani na Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Bibi Banda aliamuru uchaguzi ufutwe, akitoa sababu za kwamba uchaguzi mzima uligubikwa na  rushwa  udanganyifu na " makosa lufufu ". 

Kisha  akaamuru uchaguzi mpya kufanyika  ndani ya siku 90 lakini alisema yeye hatashiriki kuwa  mgombea ili kuhakikisha uhuru, uwazi, uaminifu na haki vinarejeshwa.

Kurudia uhesabuji.
Mahakama Kuu ilitengua  maamuzi ya Bibi Banda  baada ya DPP kulalamika na kufikisha suala hili Mahakamani na sasa Mahakama inalazimika  kuamua kama matokeo ya uchaguzi yatangazwe au uhesabuji ufanyike tena.

Tume ya Uchaguzi (MEC) imekiri kwamba yalikuwako makosa katika kupiga kura wiki iliyopita ikashauri uhesabuji wa kura urudiwe..

"Wakati niliposema  kuwa huu uchaguzi ulikuwa na ulaghai na mizengwe hakuna mtu aliamini maneno yangu. Lakini leo Najisikia kuhujumiwa na wakosoaji wangu na  nafurahi kuwa hata MEC imeona yale niliyosema na sasa suala hili liko Mahakamani ili kuamua kama uchaguzi urudiwe ama kura zihesabiwe upya," Banda aliiambia Reuters.

"Jukumu langu sasa litakuwa kuhakikisha  kwamba mapenzi ya watu yana heshimiwa na uhuru, usawa, uwazi na kuaminiana kunatimia katika  uchaguzi na hii ndiyo maana  nimetangaza kuwa  sitoshiriki kama uchaguzi utarudiwa," Banda alisema.

Banda alisifika na kupendwa  na wengi alipoingia  madarakani miaka miwili iliyopita, baada ya kifo cha Rais Mutharika, lakini umaarufu wake ulianza kuporomoka pale alipolazimika kuchukua maamuzi makali yakiwa ni pamoja na  kushusha  thamani ya fedha ya nchi yake katika kudhibiti na kuleta  utulivu wa uchumi wa nchi.

Utawala wake pia ukakumbwa na kashfa ya rushwa ya takiribani $ 15,000,000 iliyopewa jina la ' Cashgate 'Kashfa  hii iliibuka baada ya kiasi kikubwa cha fedha kugunduliwa kuwa zimeibwa kwa hila na  maafisa waandamizi wa umma , wafanyabiashara na mabenki.

Banda ,  alisema kwamba atastaafu  siasa na  kujishughulisha na shughuli za kuhudumia jamii, aidha aliongezea kwamba kwa sasa ana imani na Tume ya Uchaguzi (MEC ).
.
"Hata MEC yenyewe inakiri kuwa  yalikuwepo  mapungufu katika uchaguzi huuna  huu ni uthibitisho wa kutosha kuwezesha uhesabuji wa kura isitoshe  na wengine wana unga mkono hoja hii…. Na hili ndilo nililolisema tokea mwanzo, " Banda alijitetea.

Habari nyingine kuhusiana na hii.
====================================
Polisi wa Malawi wapiga mwandamanaji  risasi  katika  jitihada za kuzuia ghasia za waandamanaji wanaotaka  kurudiwa.uhesabuji wa kura.

Lilongwe- Malawi -Polisi wampiga mwandamanaji risasi na kufa leo siku ya Ijumaa baada ya vurugu kati ya Polisin na watu ambao walifunga barabara kwa kuchoma matairi katika kudai uhesabuji tena wa kura za uchaguzi wa Raisi Mei 20, afisa wa polisi alisema.

Taifa hilo maskini la kusini mwa Afrika lilikuwa likisubiri uamuzi wa mahakama ambao  uliotegemewa baadaye leo siku ya  Ijumaa wa Tume ya Uchaguzi Malawi ( MEC ) kuhukumu kurudiwa uchaguzi au uhesabuji wa kura upya.

Waandamanaji katika wilaya ya Mangochi, katika sehemu ya kusini mwa Malawi, walivunja madirisha ya maduka na kuchoma moto matairi kando ya barabara , na hivyo kusababisha polisi kupiga mabomu ya gesi  ya kutoa machozi na risasi za mpira kutawanya vijana hao bila mafanikio..

"Katika vurugu hii mtu mmoja ilipigwa risasi na kufa,Hili lilitokea  polisi wakijaribu kujitetea baada ya kushindwa nguvu na waandamanaji hawa waliokuwa wamejaa hasira, " afisa wa polisi Eliya Kachikuwo aliiambia Reuters.

Pia alisema maafisa wawili wa  polisi walijeruhiwa vibaya katika varangati hili..

Polisi alisema waandamanaji walikuwa wanachama wa Chama cha Watu wa Rais Joyce Banda na Lazaro Chakwera wa Malawi Congress Party , Vyama viwili ambavyo vinadai kurudiwa kwa uhesabuji wa kura.

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza