UKOO WA ALI (Shaghira ) MTHOO. MROKI NZANO



Image may contain: 1 person, outdoor

BABU HASSANI SHAGHIRA MTHOO
Eliamini Hassan ALI Salimu Ali Msangi. 
Pata mtiririko wa ukoo wa Salimu Shaghira kutoka kwa BANGALALA kwa Ufupi.
Wasangi ni uzao wa Bangalala aliyetoka huko Kenya sehemu itwayo Usangi miaka mingi iliyopita.Bangalala alizaa watoto wawili Yambii na Mnyatta.
Mnyatta yeye alirudi Kenya.Kwa hiyo habari zake hazijulikani kwa upana.
Yambii akamzaa Mang'a.Mang'a naye akamzaa Ndorokwa.
Ndorokwa akazaa mtoto akamwita jina la baba yake Mang'a. Huyu Mang'a Jr. akamzaa Mahu.
Mahu akamzaa Akavyo..Akavyo akamzaa Kiyanga.
Kiyanga akamzaa Mfuta, Mfuta akazaa watoto wawili Nzano na Setonga.
Sasa hivi nafuatilia uzao wa Setonga.
Yeyote anayejua uzao tokea setonga hadi hapi alipo anipe mtiririko huo.
Wasangi kwa sasa tiko wengi ili uweze kutambulika kuwa wewe ni nani na ni wa baba au ni wa kutoka kwa babuci yupi tunapaswa tuandike majina matatu au zaidi.Jina moja lilkifuatwa na Msang kwa mfano Abdalla Msangi, Ramadhani Msangi, au Adam Msangi halitoshi kukutambulisha kikamilifu.
Sasa, baada ya hilo angalizo, tuendelee na uzao wa Nzano.
Kwa upande wa Nzano yeye alioa wanawake wengi. Kwa jinsi hii akazaa watoto wanne. Ijumbi akiwa ni mtoto wake wa kwanza akifuata Kisarika na Komeja.
Mroki alikuwa mtoto wa nne wa Nzano, na wa mwisho kwa mke wa mwisho.
Ijumbi alizaa ukoo wa kina Senakanga ambao ni kina. Senguji na Bondera.
Komeja akawazaa Mlawa, Mramba, Idhina na Mchaimwa Huyu Mchaimwa alikuwa mwanamke uzao wake ni ukoo wa Saidi Mcholo.
Kisarika akawazaa Kisineni, Nguma,Ishiwa, Mghamba na Kinyonge Kinyonge ukoo wake ni wa kina Chakupewa.
Kisarika, Kisineni, Nguma, Mghamba koo zao ni za kufuatilia sina maeleza yake.
Tukija kwa Mroki mtoto wa Nzano wa mwisho kwa mke mdogo, huyu Mroki alimzaa mtoto mmoja akamwita Mthoo. Mthoo alizaliwa peke yake kama alivyozaliwa baba yake.
Mthoo alizaa watoto watatu Shaghira,Vichike na Nguluma.Vichike alikwa ni mwanamke na alikuwa ndiye mtoto wa kwanza kuzaliwa, akifuatiwa na Shaghira na Nguluma akiwa ni mziwanda.
Shaghira alikuwa mwiisilamu na aliitwa(Ali). Shaghira alizaa watoto wanne Hassaniakiwa wa kwanza akifuatiwa na Salimu, Ibrahimu na Selemani akiwa ndiye wa mwisho kwao.
Salimu akawazaa Ali (Shaghira Jr), Hatibu na Nauche. Huyu ni Nauche ni wa kike na ni kitinda mimba wa babu Salimu aka Kigingi
(Mbishi yakwe Namwai)
Chui aliyezaliwa na Namwai. Namwai ni mama yake.Babu Salimu.Babu Salimu alikuwa akijigamba kwa namna hiyo.
Mimi nimezaliwa na Ali (Shaghira Jr.) Salimu mtoto wa kwanza wa Salimu. Niliitwa Hassani jina la baba mkubwa wa babangu .hivyo mimi ni Hassan Jr
Huyu Hassan ambaye nimeitwa jina lake anaitwa Mthoo jina la babu yake hivyo na mimi ninatwa Mthoo wa tatu. Jina lake jingine la utani (nick name) aliitwa TILISHO.
Na mimi nina watoto Watatu Ali, Riziwani na Hatibu.
Ali ni jina la baba wa babu zangu. Alikuwa kasilimu na alikuwa imamu.
ALI mwanangu ni Ali wa tatu.
HUU NDIO MTI WA UKOO wa Salimu Ali (Shaghira)Mthoo.
KOO NYINGINE HAPO KATIKATI NI ZA KUJAZIA.
SIMULIZI hii nimesimuliwa na Babu Hassan ALi ambaye kwa jina la babu aliitwa Mthoo. Na mimi pia ni Mthoo wa tatu.
Eliamini : Msangi Nawashukuruni nyote mlio like post hii. Kwa kuwa tawi letu limeanzia kwa Nzano, nitaendeleza mtambao wa Wasangi wa tawi hili.Naomba ushirikiano wenu Wasangi wa kwa Nzano na Setonga.
Like · Reply · 1 h
Malaho Omari :Hahahaha weee kaka umenifurahisha sana mimi ni malaho mtoto wa mzee OMARI (SABUNI) wewe tumeachana hapo kwa setonga setonga alimzaa marisa na shanjarika marisa akamzaa Malaho na huyu malaho akamzaa salimu malaho JUMA malaho (babake mshare) Omari malaho...See more
Like · Reply · 1 hr
Eliamini Msangi :VYAKWA KIAMBO TUKO KARIBU SANA NAO, NAMI NITAFUATILIA.wasangi bwana wameenea sana.Omari mshare yule aliyekuwa akiishi Kwakoa.Mzee BONDERA baba yake na JUMANNE NA ERNEST BONDERA.
Chini kushoto ni babu Hassan Ali kulia babu Salimu Ali

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza