Na Mwandishi Wetu
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imepitisha uamuzi wa kutotahini tena mtihani wa somo la Dini kuanzia mwaka huu. Katika kupitisha uamuzi huo, Wizara ilikutana na taasisi za Kikristo pekee mwezi Machi mwaka huu na baadae kuwapa taarifa Bakwata juu ya maamuzi yaliyofikiwa. “Sisi tumefanya tu kupewa taarifa kuwa Serikali imepitisha uamuzi huo, lakini katika kujadili suala hilo hatukufahamishwa, Wizara ilikutana na wadau wa Kikristo pekee.” Amesema afisa mmoja wa Bakwata akielezea juu ya barua waliyoandikiwa na Kamishna wa Elimu juu ya uamuzi huo. Afisa huyo akasema kuwa wao kama Bakwata wameshangaa na kushtuka sana. Akasema kuwa pamoja na kuwa hawakushirikishwa wanakuja kupewa tu taarifa, lakini wanashangaa pia kwa sababu hata walipopewa taarifa na Kamishna wa Elimu, wameambiwa jambo hilo liwe siri.

Jambo hili linafanywa “SIRI, je Serikali inataka Waislamu wasiambiwe? Kwanini? Kuna agenda gani? Amehoji afisa huyo ambaye hata hivyo hakutaka kutaja jina lake akisema kuwa yeye sio msemaji wa Bakwata. Awali taarifa juu ya kikao cha Wakristo na Wizara juu ya mitihani ya dini, zilianza kuvuja kupitia kwa Wakristo waliohudhuria ambao walipokutana na wadau kutoka upande wa Waislamu waliwalaumu ni kwa nini hawakuhudhuria wakasaidiana kupinga uamuzi huo wa Serikali. Hata hivyo, wadau hao kutoka Islamic Education Panel waliwafahamisha wadau hao wa Kikristo kuwa wao walikuwa hawakupewa taarifa.

Kufuatia kuvuja kwa taarifa hizo, baadhi ya wajumbe wa Islamic Education Panel walifuatilia jambo hilo Bakwata wakidhani kuwa huenda Bakwata wao walipewa taarifa. Hata hivyo, maofisa wa Bakwata wakasema kuwa nao wanasikia tu, hawakualikwa. Kwa muda mrefu Serikali imekuwa ikitahini masomo ya Dini ya Kiislamu (Maarifa ya Uislamu) na Kikristo (Divinity) katika mitihani ya kidato cha nne na sita na pia katika Mafunzo ya Ualimu ngazi ya Cheti na Stashahada. Kwa upande wa Maarifa ya Uislamu, Wizara imekuwa ikishirikiana na Islamic Education Panel katika kuandaa mihutasari na mitihani kwa ngazi zote hizo.

Vitabu vya mihutasari hiyo, kwa ngazi zote, katika jalada vimewekwa nembo ya Serikali na ile ya Islamic Education Panel na kusainiwa na Kamishana wa Elimu. Hata hivyo, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, haikuwaita IEP katika kupitisha uamuzi huo mkubwa na wenye athari kubwa kwa vijana wa Kiislamu na vyuo vya Kiislamu. Hivi sasa Vyuo Vikuu kama kile cha Waislamu Morogoro (MUM), pamoja na wanafunzi wa kozi nyingine, huchukua wanafunzi waliomaliza kidato cha sita na kufaulu Somo la Islamic Knowledge kwa ajili ya kuchukua kozi ya Sheria na Sharia kwa pamoja. Aidha, huchukua pia wanafunzi hao kwa ajili ya kozi ya Masomo ya Dini na Ualimu, yaani BA Islamic Studies and Education. Kwa upande mwingine, Chuo Kikuu cha Elimu Zanzibar (Chukwani) na kile cha Tunguu, navyo vinachukua wanafunzi waliomaliza kidato cha sita na kufaulu somo la Maarifa ya Uislamu kwa ajili ya kozi zao mbalimbali. Vipo pia vyuo vikuu vya Mbale Uganda, Sudan, Uturuki, Malaysia na sehemu nyingine ambapo wana kozi zinazohitaji somo la Maarifa ya Uislamu kama vile Islamic Banking.

Kwa uamuzi huu wa Serikali, ina maana kuwa sasa itakuwa vigumu kwa MUM na Chukwani kupata wanafunzi wenye sifa kwa hiyo huenda vikalazimika kufuta kozi hizo. Hii maana yake ni kuwa uamuzi huu unapunguza idadi ya wanafunzi wa Kiislamu wanaokuwa na sifa za kupata elimu ya juu. “Kinachosikitisha ni kuwa Serikali imeamua kukaa na Wakristo pekee kupitisha maamuzi mazito kama haya bila kujali athari yake kwa vijana wa Kiislamu na taasisi za Kiislamu nchini.” Amesema mjumbe mmoja wa Islamic Education Panel akizungumzia suala hilo. “Hii ni dharau iliyopitiliza kiwango, Serikali inachukuaje maamuzi kama haya bila kujali kuwa kuna shule za Kiislamu na Vyuo vya Ualimu vya Kiislamu pamoja na Vyuo Vikuu ambavyo vinategemea kupata wanafunzi kutokana na wanafunzi wanaomaliza kidato cha sita wenye somo la Maarifa ya Uislamu?” Amesema mjumbe huyo wa Islamic Education Panel ambaye hata hivyo hakutaka kutajwa jina lake gazetini.

“Kama Serikali imeona kuna mantiki kujitoa katika kutahini somo hili, kwa nini ifanye kinyemela? Kwa nini isiwashirikishe wadau husika ili kujua, ni utaratibu gani mwingine utafanyika ili vyuo vya Kiislamu vilivyopo visiathirike? Kwa nini wasikae pamoja na Panel? Mbona waliwaita Wakristo? Kitu gani kiliwafanya wakwepe kuwaita Waislamu, ni dharau, UDINI, au kuna agenda ya siri?”

Mdau mmoja wa Kikristo aliyekuwa katika kikao hicho cha Machi kati ya Serikali na wadau wa Elimu wa Kikristo alipoulizwa kuwa katika kikao hicho Serikali imetoa hoja gani ya kufuta mtihani huo alisema kuwa, hakuna jambo lililoelezwa la kujenga hoja madhubuti, lakini yeye binafsi anadhani ni kutokana na masuala ya Waislamu toka walipopinga matokeo ya Islamic mpaka ikabidi Baraza la Mitihani liyabadili. Wajumbe wa Islamic Education Panel wanasema kuwa, wakati Waislamu wametimiza matakwa yote ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya kuwa na Mihutasari na vitabu kwa ngazi zote, Wakristo hawakuwa wametimiza matakwa hayo, hawakuwa hata na mihutasari, lakini somo lao lilikuwa likitahiniwa.

Hata hivyo, akasema, hao hao ambao hawakuwa wametimiza matakwa ya Wizara na Baraza la Mitihani, ndio walioitwa kupitisha uamuzi wa Serikali kujitoa katika kutahini mtihani huo. “Waislamu wakilalamika kuwa kuna ubaguzi, udhalilishaji, uonevu na udini, wanaambiwa wanafanya uchochezi, hivi Serikali inaweza kukaa na Waislamu pekee na kufanya maamuzi makubwa yenye kugusa masilahi ya Kanisa Katoliki na Wakristo wote, halafu ifanye tu kuwapelekea taarifa Baraza la Maaskofu juu ya maamuzi hayo?” Alihoji. Wachambuzi wa masuala ya kidini na kijamii nchini wanasema kuwa huenda Serikali imeamua kujitoa katika suala hili ili ipate fursa ya kuweka mkakati mwingine wa kuibuka na somo la dini mseto baada ya kukwama huko nyuma. Hata hivyo wengine wanasema kuwa hii ni moja tu ya mikakati ya kupunguza idadi ya vijana wa Kiislamu wenye sifa za kujiunga na vyuo vikuu.

Wengine wakakumbusha kuwa zilipoanzishwa shule za kwanza za seminari za Kiislamu, Serikali ilitangaza kuwa shule hizo sio shule zinazotambulika. Ni Madrasa. Kwa hiyo wanafunzi wake wakimaliza kidato cha nne wasingepatiwa nafasi za kusoma kidato cha tano katika shule za Serikali. Na kwamba kwa wale watakaomaliza kidato cha sita, wasingechaguliwa kuingia vyuo vikuu na vyuo vingine vya Serikali. Kwa vile isingewezekana kutangaza kuwa wasiotakiwa ni Waislamu pekee, ilibidi tangazo liguse shule zote pamoja na seminari za Kikristo.

Hata hivyo, baadae alilazimka wenyewe kuondoa tena kimya kimya sera hiyo kabla haijafanyiwa kazi, baada ya kuona kuwa watakao athirika zaidi ni vijana wa Kikristo kwa sababu ni taasisi za Kikristo zilizokuwa na shule nyingi za seminari. Ni kwa sababu ya matukio kama hayo, baadhi ya wachambuzi wanasema kuwa huenda kuna agenda ya siri inayowalenga Waislamu na ndio maana waliitwa Wakristo pekee ili waelimishwe kuwa wawe radhi kutoa muhanga mtihani wa ‘Divinity’. 

Kwa upande mwingine huenda hawakuitwa Waislamu kwa kuhofiwa kuwa wangehoji mambo ambayo yasingeweza kupatiwa majibu moja likiwa ni utaratibu gani umeandaliwa kuhakikisha kuwa MUM, Chukwani na vyuo vingine vya Kiislamu vyenye kozi za Islamic Studies, Shariah na Islamic Banking, vitapata wanafunzi kulingana na vigezo vya Mamlaka ya Vyuo Vikuu- Tanzania Commission for Universities (TCU). Habari kutoka ndani ya Bakwata na Islamic Education Panel zinasema kuwa taarifa kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi juu ya suala hilo, imeeleza kuwa nao Wizara wamefanya kupewa maelekezo na Katibu Mkuu Kiongozi, Ikulu.

Na kwamba Wizara ilitakiwa kukaa na wadau, kwa maana ya taasisi za kidini kuangalia suala hilo. Hata hivyo, haikuweza kufahamika kuwa uamuzi wa kutokuwashirikisha Waislamu na badala yake kukaa na Wakristo pekee, ilikuwa ni maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi au ulikuwa uamuzi wa Kamishna wa Elimu. Wadadisi wengine wanasema kuwa jambo hili limetokea Baraza la Mitihani (NECTA) na kwamba kama ambavyo Baraza hilo liliona umuhimu wa kuajiri Mchungaji wa kutizama masilahi ya wanafunzi wa Kikristo na kugoma kuajiri Muislamu, ndio mtindo huo huo umetumika katika kuita kikao cha Wizarani. Kutokana na hali hiyo, Waislamu kupitia taasisi zao, wamepanga kumuona Katibu Mkuu Kiongozi kupata ufafanuzi juu ya suala hilo.

Na kwa kuwa suala hili linagusa masilahi ya Waislamu wote nchini, litafanyiwa taratibu za kujadiliwa na kupitishwa maamuzi ya pamoja. Hadi jana tukienda mitamboni juhudi za kuwapata wahusika Wizara ya Elimu na NECTA kuzungumzia suala hili, hazikuweza kufanikiwa.
..
Taarifa ya matokeo ya uchaguzi katika vijiji vya Mlandizi leo tr 15.10.2017 kama ifuatavyo
1.kitongoji gwata mjini. Waliojiadikisha 248. WalioPiga kura 161. iriyo haribika 1. Ccm 151. Chadema 9.
2.kijiji lukenge. Waliojiandikisha 487. Walio piga kura 436. Zilizo haribika 3. Ccm 333. Chadema 100
3.Kijiji Gumba. Waliojiandikisha 290. Walio piga kura 250.zilizo haribika 4. Ccm 220. Chadema 26.
4. Kitongoji Cha Midizini ZILIZOPIGWA 143,ZILlZO HARIBIKA 3,CCM 78,CUF 62,WALIOANDIKISHWA 156.
5. Mwenyekiti wa kijiji Misufini, waliojiandikisha 233, waliopiga kura 222,zilizoharibika 2,CCM 127 na CHADEMA 91
6. Ngeta: Waliojiandikisha 354: waliopiga kura 314 zilizoharbika 2 CCM 188 CHADEMA 124
7. Kitongoji cha Mkarambati Waliojiandikisha 62 waliopiga kura 60 ccm Kura 22 chadema kura 38. 

Taarifa hii toka kwa 
Beatrice Condrad TANURU LA FIKIRA
MWANAMME NI KAZI
Katika utafiti wa hivi karibuni, watafiti wamegundua kwamba, wanawake wanawapenda wanaume wasio waoga na mashujaa kuliko wale waoga. Ushujaa wa wanaume ni kigezo kikubwa kwa wanawake kuwapenda marafiki wa kiume wa muda mrefu na muda mfupi. 

Hii inamaanisha kwamba katika urafiki wa kawaida na wa kimapenzi na wa kindoa, wema au ukarimu ulionekana kwamba ni kigezo cha kawaida tu na sio kipaumbele chao.

Tukirudi kwa mababu zetu wa kale walioishi mapangoni, wanawake waliwapenda wanaume shujaa ambao wangeweza kujitoa muhanga kuwalinda wao na watoto wao. Mwanaume ambaye alikuwa na uwezo wa kujitoa muhanga alionekana kuwa na uwezo wa kuwinda bila hofu na kuzama porini kutafuta chakula kwa Ajili ya familia au kutafuta dawa kwa ajili ya matibabu kwa familia yake.

Kikubwa hapa ni ulinzi na usalama. Na hili linawafanya wanawake wengi kuwapenda mabaunsa kwa sababu hih hii ya ulinzi na usalama
Mwanaume mwenye nazo anaonekana kupendwa lakini hapa swala si fedha yake, bali anaonwa kama ndiye anayeweza kuilinda familia. Ukikuta wanawake wanavutiwa na wanaume wenye fedha, usishangae, kwani bado wanaongozwa na  haja yao kuu ya  kuhakikishiwa usalama wao.

Kwa kifupi ni kwamba kinachotafutwa na wanawake ni  amani nausalama.

Siku hizi  fedha imechukua nafasi katika kujihakikishia usalama wetu. Kila kitu siku hizi ni pesa na ndio maana wanawake kwa dhana ile ile ya kujihakikishia usalama wanavutiwa na wanaume wenye nazo.

Sio kwa sababu ya tamaa...... La hasha, ni kutaka kuwa na uhakika na maisha yake na familia yake.
Mwanamume akikosa sifa ya fedha ataangaliwa kwa ujasiri  na uchakarikaji.Kwa haya mwanamke anajua kwamba kwa kushirikiana naye mbeleni maisha yatakuwa mazuri na salama.
Ikitokea kwa mfano kaolewa na mwanaume mzigo au siku hizi huwaita "Dead alive" au mwanaume suruali, jukumu la kutafuta hulishika mwenyewe kwa sababu hamna jinsi na mara nyingi hufanikiwa kuzikamata kwa sababu anafanya hivyo kwa nia na dhamira ya kujihakikishia usalama.
Kama vile wanaume wanavyokosea kuoa kwa kutopiga hesabu zao vizuri katika kuoa vivo hivyo wanawake nao hukosea kwa kudanganyika na zile sifa za mwanaume za muda mfupi bila kuchunguza vizuri zaidi. 

Wapo ambao wakigundua kwamba mwanaume aliyeolewa naye ni mvivu na asiyejali familia anafungasha na kuondoka, lakini wapo ambao wanatafuta suluhu na kuamua kushika hatamu za kuendesha nyumba hawa ni wale wanaoogopa kufanya makosa kwa mara ya pili yaani kuondoka na kuangukia kwa mwanaume mwingine mwenye sifa zisizopendeza. Hawa wanakubali matokeo na kuamua kusimama kama wao, hawayumbishwi na huwakubali wenzi wao kama walivyo.

Wanawake wa aina hii mara nyingi kufanikiwa sana tofauti na wale wanaojipweteka na kubaki wakilalamika. Lakini naomba niseme kuwa wanawake kwa kiasi kikubwa ni mashujaa hawawezi kukaa na kuangalia familia ikianguka kwa sababu mwanaume hawawajibiki. Wengi sana tena kiasi cha kutosha husimama na kushika nyumba kwani wanajua kwamba nyumba ikianguka mara nyingi lawama huwaendea wao.

Pia mwanamke huvutiwa na mwanaume anayejali usalama wa wazazi na ndugu  zake Mwanamke yuko tayari kumpenda mume mwingine nje ya ndoa kama huyu mume ataonesha  upekee katika kuwa chukua wazazi wake.

Kwa mfano wapo wanaume wengi hali zinapokuwa ngumu huzikimbia familia zao na kuzitelekeza hata kwa miaka kadhaa, lakini wakirudi wanakuta familia ipo mbali kimandeleo na watoto wana hali nzuri. Hao ndiyo huitwa wanawake wa shoka. Lakini maendeleo hay0 huwa hayaji hivi hivi, yuko mwanamume aliyependwa badala ya aliyeikimbia familia.

Kwa hiyo swala la uelewa,umaridadi, utanashati katika siyo sifa zinazotazamwa na wanaume bali ni ulinzi na upendo, 

Kwa wanaume vigezo ni utii, na matunzo mazuri. Vitu hivi kwao ni muhimu katika swala zima la kutafuta mwenza. 
Heri ya Pasaka. 
UJUMBE MZITO WA PAPA FRANCIS
Hakuna familia isiyo na mapungufu. Hatuna wazazi wasio na mapungufu, sisi pia si wakamilifu, hatuoi au kuolewa na mtu asiye na mapungufu, kadhalika watoto wetu nao si wakamilifu. Tunayo manung'uniko au malalamiko kila mmoja dhidi ya mwenzake. Tumevunjana moyo na kukatishana tamaa. Kwa hiyo, hakuna ndoa iliyokamilika wala familia iliyoboreka bila kuwa na mazoea au utamaduni wa kusameheana.

Msamaha ni nguzo au msingi wa utulivu wa akili na uhai wa roho zetu. Kama hakuna msamaha, familia inakuwa uwanja wa migogoro na mlipuko wa ugomvi. Panapokosekana msamaha, familia inaugua. Msamaha unahuisha moyo, kwa kusafisha fikra na kuufanya moyo kuwa huru. Binadamu asiyesamehe hana amani moyoni na wala hana urafiki au muunganiko na Mungu.

Maumivu ni sumu inayodhuru na kuua. Hebu kiponye kidonda hicho cha moyo endapo kuna dalili za kujiumiza. Mtu asiyesamehe anajisababishia mwenyewe ugonjwa wa mwili, kiakili na kiroho. Ndiyo maana familia inapaswa kuwa sehemu ya uhai na si kifo; eneo la uponyaji na sio mahali pa magonjwa; jukwaa la msamaha na si la uovu. Msamaha huleta furaha pale uchungu ulipoleta maumivu; huleta uponyaji hata pale ambapo maumivu yalisababisha magonjwa.

Ujumbe huu wa Baba Mtakatifu umfikie kila mmoja wetu leo katika familia yake. Leo basi tuutafakari ujumbe huo muhimu.

Ewe  Mwenyezi Mungu Tusamehe makosa yetu tunayoyajua na yale tusiyoyajua, Aamin.

Muhimu:Kauli hii haimlengi mtu fulani , bali ni mafundisho kwa  mimi mwenyewe  na jamii yote kwa ujumla.
METHALI MIA SITA NA KUMI (610)
1. Aanguaye huanguliwa.
2. Asiye sikia la mkuu, huvunjika guu.
3. Abebwaye hujikaza.
4. Adhabu ya kaburi aijuae maiti.
5. Adui aangukapo, mnyanyue.
6. Adui mpende.
7. Adui wa mtu ni mtu.
8. Afadhali ya Musa kuliko ya Firauna.
9. Ahadi ni deni.
10. Ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.
11. Akiba haiozi.
12. Akili ni mali.
13. Akili ni nywele kila mtu ana zake.
14. Akili nyingi huondowa maarifa.
15. Akutukanae hakuchagulii tusi.
16. Akipenda chongo huita kengeza.
17. Akufaae kwa dhiki, ndiye rafiki.
18. Akufanyiaye ubaya, mlipe wema.
19. Akupaye kisogo si mwenzio.
20. Akutendaye mtende, mche asiyekutenda.
21. Alisifuye jua, limeuangaza.
22. Aliye juu msubiri chini.
23. Aliye kando, haangukiwi na mti.
24. Aliye kupa wewe kiti (kibao) ndiye aliye nipa mimi kumbi.
25. Aliye kutwika, ndiye atakaye kutua.
26. Akufukuzae hakwambii toka.
27. Aliyekupa mkeka ndiye aliyenipa kumbesa.
28. Amani haipatikani mpaka kwa ncha ya upanga.
29. Ana hasira za mkizi.
30. Anayekuja pasi na hodi, huondoka bila ya kuaga.
31. Angurumapo simba, mcheza ni nani?
32. Aninyimaye mbazi kanipunguzia mashuzi.
33. Apewaye ndiye aongezwaye.
34. Anaejipiga mwenyewe, halii.
35. Asifuye mvuwa imemnyea.
36. Asiye kubali kushindwa si mshindani.
37. Asiye kujua, hakuthamini.
38. Asiye kuwapo na lake halipo.
39. Asiye lelewa na mamae hulelewa na ulimwengu.
40. Asiye na mengi, ana machache.
41. Asiye uliza, hanalo ajifunzalo.
42. Asiyejua maana, haambiwi maana.
43. Atangaye na jua hujuwa.
44. Atangazaye mirimo, si mwana wa ruwari (Liwali).
45. Atekaye maji mtoni hatukani mamba.
46. Avumaye baharini papa kumbe wengi wapo.
47. Baada ya dhiki faraja.
48. Bahari hailindwi.
49. Bamba na waume ni bamba, hakuna bamba la mume.
50. Bandu bandu huisha gogo.
51. Baniani mbaya, kiatu chake dawa.
52. Bendera hufuata upepo.
53. Biashara asubuhi.
54. Bilisi wa mtu ni mtu.
55. Bora kinga kuliko tiba.
56. Bora lawama kuliko fedheha.
57. Bora mchawi kuliko fitina.
58. Biashara asubuhi.
59. Bora nusu shari kuliko shari kamili.
60. Bwawa limeingia ruba.
61. Cha mtu mavi.
62. Chaka la samba, halilali nguruwe.
63. Chamlevi huliwa na mgema.
64. Chanda chema huvikwa pete.
65. Chelewa chelewa, utakuta mtoto si wako.
66. Choko mchokoe pweza, binaadamu hutomuweza.
67. Chombo cha kuzama hakina usukani.
68. Chovya - chovya yamaliza buyu la asali.
69. Chui hakumbatiwi.
70. Chururu si ndo ndo ndo.
71. Dalili ya mvua mawingu.
72. Damu nzito kuliko maji.
73. Daraja livuke ulifikapo.
74. Dawa ya moto ni moto.
75. Daraja ukilibomoa, ujue kuogelea.
76. Dau la mnyonge haliendi joshi, likienda joshi ni matakwa ya Mungu.
77. Dawa ya moto ni moto.
78. Donda ndugu halina dawa.
79. Dua ya kuku haimpati mwewe.
80. Fadhila huna, hata hisani hukumbuki?
81. Fadhila ya nyuki ni moto.
82. Fadhila ya punda ni mateke (mashuz)
83. Fahari ya macho haifilisi duka.
84. Farasi hamuwawezi, tembo mtawalishani?
85. Fata nyuki ule asali.
86. Fimbo ya mbali haiui nyoka.
87. Fumbo mfumbe mjinga, mwerevu huligangua.
88. Funika kombe mwanakharamu apite.
89. Ganda la mua la jana, chungu kaona kivuno.
90. Gome la udi, si la mnuka uvundo.
91. Haba na haba, hujaza kibaba.
92. Haki ya mtu hailiki.
93. Hakuna masika yaso mbu.
94. Hakuna msiba usio na mwenziwe.
95. Hakuna siri ya watu wawili.
96. Hakuna ziada mbovu.
97. Hala hala mti na macho.
98. Hamadi ni ilio kibindoni, na silaha ni iliyo mkononi.
99. Hapana marefu yasio na mwisho.
100. Haraka haraka haina baraka.
101. haraka haraka haina baraka.
102. Haramu yako halali kwa mwenzio.
103. Hasidi hasada.
104. Hasidi mbaya.
105. Hasira, hasara.
106. Hatua ndefu hufupisha mwendo.
107. Hauchi hauchi, unakucha.
108. Hayawi hayawi, mara huwa.
109. Heri kufa macho kuliko kufa moyo.
110. Heri kujikwa kidole kuliko ulimi.
111. Heri nitakula na nini?, kuliko nitakula nini?
112. Heri ya marama kuliko kuzama.
113. Hiari ya shinda utumwa.
114. Hogo halihogoki mpaka kwa hogo jenziwe.
115. Hucheka kovu asiye kuwa na jeraha.
116. Ila ya kikwapa, kunuka pasipo kidonda.
117. Yaliyoopita si ndwele, ganga yajayo.
118. Iliyo jaa ndiyo ipunguzwayo.
119. Imara ya jembe kaingojee shambani.
120. Jambo usilolijua, usiku wa giza.
121. Jina jema hungara gizani.
122. Jini likujualo halikuli likakwisha.
123. Jino la pembe si dawa ya pengo.
124. Jitihada haiondoi kudura.
125. Jitihadi haiondoi kudura.
126. Jogoo la shamba haliwiki mjini.
127. Jungu kuu, halikosi ukoko.
128. Jununu fununu.
129. Kafiri akufaaye, si muislamu asiye kufaa
130. Kafiri akufaye si Isilamu asiyekufa.
131. Kama hujui kufa,tazama kaburi.
132. Kama wewe wasema cha nini, mwezio asema nitakipata lini.
133. Kamba hukatika pabovu.
134. Kanga hazai ugenini.
135. Kawaida ni kama sheria.
136. Kawia ufike.
137. Kazi mbaya siyo mchezo mwema.
138. Kelele za chura hazimzuwii ng'ombe kunywa maji.
139. Kelele za mlango haziniwasi usingizi (Kelele za mlango hazimuudhi mwenye nyumba)
140. Kenda karibu na kumi.
141. Kesho kesho, kesho kiama.
142. Kiburi si maungwana.
143. Kibuzi na kibuzi hununua jahazi.
144. Kichango kuchangizana.
145. Kidole kimoja hakivunji chawa.
146. Kikulacho ki nguoni mwako.
147. Kikushindacho kukila usikitie ila.
148. Kila chombo kwa wimblile.
149. Kila mbwa hubwekea mlangoni kwao.
150. Kila mlango na ufunguwo wake.
151. Kila mtoto na koja lake.
152. Kila mtu huzikwa na kaburi lake.
153. Kila mtu na bahati yake.
154. Kila mwamba ngoma ,ngozi huivuta kwake.
155. Kila mtu hulilia mamae.
156. Kila ndege huruka kwa ubawa wake.
157. Kila shetani na mbuyu wake.
158. Kilimia kikizama kwa jua, huzuka kwa mvua, na kikizama kwa mvua, huzuka kwa jua.
159. Kilio huanza mfiwa ndipo wa mbali wakaingia.
160. Kimya kingi kina mshindo mkubwa.
161. Kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
162. Kingiacho mjini si haramu.
163. Kinyozi hajinyoi.
164. Kinywa ni jumba la maneno.
165. Kipendacho moyo dawa.
166. Kipofu hasahau mkongojo wake.
167. Kipya kinyemi ingawa kidonda.
168. Kisebusebu na kiroho papo.
169. Kisokula mlimwengu, sera nale.
170. Kisokula mlimwengu,sera nale.
171. Kisu kimenifika mfupani.
172. Kitanda usicho kilalia hukijui kunguni wake.
173. Kitumbua kimeingia mchanga.
174. Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua.
175. Kiwi cha yule ni chema cha; hata ulimwengu uwishe.
176. Kizuri chajiuza kibaya chajitembeza.
177. Konzi ya maji, haifumbatiki.
178. Konzo ya maji haifumbatiki.
179. Kosa moja haliachi mke.
180. Kozi mwandada, kulala na njaa kupenda.
181. Kuagiza kufyekeza.
182. Kuambizana kuko kusikilizana hapana.
183. Kucha M'ngu si kilemba cheupe.
184. Kuchamba kwingi, kuondoka na mavi.
185. Kufa kufaana.
186. Kufa kwa jamaa, harusi.
187. Kufa kwa mdomo,mate hutawanyika.
188. Kufanaya kosa sio kosa, kosa ni kurudia kosa.
189. Kuishi kwingi, kuona mengi.
190. Kujikwa si kuanguka,bali ni kwenda mbele.
191. Kujikwaa si kuanguka, bali ni kwenda mbele.
192. Kukopa harusi kulipa matanga.
193. Kukopa harusi, kulipa matanga.
194. Kuku havunji yai lake.
195. Kuku mgeni hakosi kamba mguuni.
196. Kula kutamu ,kulima mavune.
197. Kulea mimba si kazi kazi kulea mwana.
198. Kukopa harusi, kulipa matanga.
199. Kumuashia taa kipofu ni kuharibu mafuta.
200. Kunako matanga kume kufa mtu.
201. Kunguru mwoga hukimbiza mbawa zake.
202. Kupanda mchongoma, kushuka ndio ngoma.
203. Kupata si werevu, na kukosa si ujinga.
204. Kupoteya njia ndiyo kujua njia.
205. Kurambaramba ndio kula, kunenepa kwake Mola.
206. Kusikia si kuona.
207. Kutangulia si kufika.
208. Kutoa ni moyo usambe ni utajiri.
209. Kutu kuu ni la mgeni.
210. Kuugua sio kufa.
211. Kuvuja kwa pakacha nafuu ya mchukuzi.
212. Kuzima koleo si mwisho wa uhunzi.
213. Kwa mwoga huenda kicheko na kwa shujaa huenda kilio.
214. Kweli ilio chungu, si uongo ulio mtamu.
215. Kwenda mbio siyo kufika.
216. Kwenye miti hakuna wajenzi.
217. La kuvunda halina rubani.
218. La kuvunda halina ubani.
219. Lake mtu halimtapishi bali humchefua.
220. Leo kwako, kesho kwa mwenzio.
221. Leo ni leo asemayo kesho ni mwongo.
222. Liandikwalo ndiyo liwalo.
223. Lila na fila hazitangamani.
224. Lipitalo, hupishwa .
225. Lisemwalo lipo,ikiwa halipo laja.
226. Lisilo na mkoma, hujikoma lilo.
227. Lisilokuwapo moyoni, halipo machoni.
228. Maafuu hapatilizwi.
229. Macho hayana pazia.
230. Mafahali wawili hawakai zizi moja.
231. Maiti haulizwi sanda.
232. Maji hayapandi mlima.
233. Maji hufuata mkondo.
234. Maji ukiyavuliya nguo huna budi kuyaoga.
235. Maji usiyoyafika hujui wingi wake.
236. Maji ya kifuu, bahari ya chungu.
237. Maji yakijaa hupwa.
238. Maji yakimwagika hayazoleki.
239. Maji yamenifika shingoni.
240. Majuto ni mjukuu.
241. Mali ya bahili huliwa na wadudu.
242. Mama ni mama, hata kama ni rikwama.
243. Mama nipe radhi kuishi na watu kazi.
244. Mambo kunga.
245. Manahodha wengi chombo huenda mrama.
246. Maneno makali hayavunji mfupa.
247. Maneno mazuri humtowa nyoka pangoni.
248. Maneno si mkuki.
249. Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichika.
250. Masikini akipata matako hulia mbwata.
251. Masikini haokoti,akiokota huambiwa kaiba.
252. Masikini na mwanawe tajiri na mali yake.
253. Maskini hana kinyongo.
254. Mavi usioyala, wayawingiani kuku?
255. Mavi ya kale hayanuki.
256. Mbinu hufuata mwendo.
257. Mbio za sakafuni huishia ukingoni.
258. Mbiu ya mgambo ikilia kuna jambo.
259. Mchagua jembe si mkulima.
260. Mchagua nazi hupata koroma.
261. Mchagua nazi si mfuaji.
262. Mchakacho ujao,halulengwi na jiwe.
263. Mchama ago hanyeli,huenda akauya papo.
264. Mchamba kwingi mara ujitia dole.
265. Mcheka kilema hafi bila kumpata.
266. Mchele mmoja mapishi mengi.
267. Mchelea mwana kulia hulia yeye..
268. Mcheza hawi kiwete, ngoma yataka matao.
269. Mcheza kwao hutuzwa.
270. Mcheza na tope humrukia.
271. Mchezea mavi, hayaachi kumnuka.
272. Mchezea zuri, baya humfika.
273. Mchimba kisima hungia mwenyewe.
274. Mchonga mwiko hukimbiza mkono wake.
275. Mchuma janga hula na wakwao.
276. Mchumia juani,hulia kivulini.
277. Mdharau biu, hubiuka yeye.
278. Mdharau mwiba humchoma.
279. Meno ya mbwa hayaumani.
280. Mfa maji haachi kutapatapa.
281. Mfa maji hukamata maji.
282. Mficha uchi hazai.
283. Mfinyazi hulia gaeni.
284. Mfuata nyuki hakosi asali.
285. Mfukuzwa kwao hana pakwenda.
286. Mgaagaa na upwa hali ugari kande.
287. Mganga hajigangi.
288. Mgema akisifiwa tembo hulitia maji.
289. Mgeni ni kuku mweupe.
290. Mgeni njoo mwenyeji apone.
291. Mgomba haushindwi na mkunguwe.
292. Mgonjwa haulizwi uji.
293. Miye nyumba ya udongo, sihimili vishindo.
294. Mjinga akierevuka mwerevu yupo mashakani.
295. Mjinga mpe kilemba utamuona mwendowe.
296. Mjumbe hauawi.
297. Mkaidi hafaidi mpaka siku ya idi.
298. Mkamatwa na ngozi ndiye mwizi.
299. Mkamia maji hayanywi.
300. Mkamia maji hayanywi.
301. Mkataa la mkuu huvunjika guu.
302. Mkataa wengi ni mchawi.
303. Mkataa ya Musa hupata ya Firauna.
304. Mke ni nguo, mgomba kupalilia.
305. Mkono moja hauchinji ng'ombe.
306. Mkono moja haulei mwana.
307. Mkono mtupu haulambwi.
308. Mkono usioweza kuukata,ubusu.
309. Mkosa kitoweo humangiria.
310. Mkuki kwa nguruwe, kwa mwanadamu uchungu.
311. Mkulima ni mmoja walaji ni wengi.
312. Mla cha mwenziwe na chake huliwa.
313. Mla cha uchungu na tamu hakosi.
314. Mla kuku wa mwenziwe miguu humwelekea.
315. Mla mbuzi hulipa ngombe.
316. Mla mla leo mla jana kala nini?
317. Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
318. Mlala na maiti haachi kulia lia.
319. Mlenga jiwe kundini hajui limpataye.
320. Mlimbua nchi ni mwananchi.
321. Mnyamaa kadumbu.
322. Mnywa maji kwa mkono mmoja,Kiu yake i pale pale.
323. Moja shika, si kumi nenda urudi.
324. Moto hauzai moto.
325. Mpanda farasi wawili hupasuka msamba.
326. Mpanda ngazi hushuka.
327. Mpanda ovyo hula ovyo.
328. Mpemba akipata gogo hanyii chini.
329. Mpemba hakimbii mvua ndogo.
330. Mpende akupendae asiyekupenda achana naye.
331. Mpiga ngumi ukuta huumiza mkonowe.
332. Mpofuka ukongweni,hapotewi na njia.
333. Msafiri kafiri.
334. Msafiri masikini ajapokuwa sultani.
335. Msasi haogopi mwiba.
336. Msema kweli hukimbiwa na rafiki zake.
337. Msema pweke hakosi.
338. Mshika kisu, hashiki makalini.
339. Mshale kwenda msituni haukupotea.
340. Mshoni hachagui nguo.
341. Msi bahati, habahatishi.
342. Msi mbele, hana nyuma.
343. Msishukuru mja, hamshukuru Molawe.
344. Msitukane wagema na ulevi ungalipo.
345. Msitukane wakunga na uzazi ungalipo.
346. Mstahimilivu hula mbivu.
347. Mtaka cha mvunguni sharti ainame.
348. Mtaka lake hasindwi.
349. Mtaka nyingi nasaba hupata mwingi msiba.
350. Mtaka unda haneni.
351. Mtaka uzuri hudhurika.
352. Mtaka yote hukosa yote.
353. Mtegemea nundu haachi kunona.
354. mtegemea nundu, haachi konona.
355. Mtego bila ya chambo, haunasi.
356. Mtembezi hula miguu yake.
357. Mteuzi heshi tamaa.
358. Mti hauwendi ila kwa nyenzo.
359. Mtondoo haufi maji.
360. Mtoto akililia wembe mpe.
361. Mtoto umleyavyo ndivyo akuavyo.
362. Mtoto wa nyoka ni nyoka.
363. Mtu hakatai mwito,hukata aitwalo.
364. Mtu hujikuna ajipatapo.
365. Mtu huulizwa amevaani ,haulizwi amekulani.
366. Mtumai cha ndugu hufa masikini.
367. Mtumi wa kunga haambiwi maana.
368. Mtumikie kafiri upate mradi wako.
369. Mtupa jongoo hutupa na mti wake.
370. Muhitaji khanithi walau kana rijaali.
371. Muiba yai leo kesho hua mwizi wa ng'ombe.
372. Mume wa mama ni baba.
373. Mungu hamfichi mnafiki.
374. Mungu si asumani.
375. Muonja asali haonji mara moja.
376. Muuza sanda, mauti kwake harusi.
377. Mvua nguo, huchutama.
378. Mvumbika changa hula mbovu.
379. Mvumbika pevu hula mbivu na mvumbika changa hula mbovu.
380. Mvungu mkeka.
381. Mvunja nchi ni mwananchi.
382. Mvuvi ajuwa pweza alipo.
383. Mwacha asili ni mtumwa.
384. Mwamba na wako hukutuma umwambiye.
385. Mwamini Mungu si mtovu.
386. Mwana maji wa kwale kufa maji mazowea.
387. Mwana mkuwa nawe ni mwenzio kama wewe.
388. Mwana simba ni simba.The child of lion is a lion.
389. Mwana wa kuku hafunzwi kuchakura.
390. Mwana wa mtu ni kizushi, akizuka, zuka naye.
391. Mwanga mpe mtoto kulea.
392. Mwangaza mbili moja humponyoka.
393. Mwanzo kokochi mwisho nazi.
394. Mwanzo wa chanzo ni chane mbili.
395. Mwanzo wa ngoma ni lele.
396. Mwapiza la nje hupata la ndani.
397. Mwekaji kisasi haambiwi mwerevu.
398. Mwenda bure si mkaa bure,huenda akaokota.
399. Mwenda mbio hujikwa kidole.
400. Mwenda omo na tezi marejeo ni ngamani.
401. Mwenda pole hajikwai.
402. Mwenda wazimu hapewi panga.
403. Mwenda wazimu hapoi, bali hupata nafuu.
404. Mwenye haja hwenda chooni.
405. Mwenye kelele hana neno.
406. Mwenye kovu usidhani kapowa.
407. Mwenye kubebwa hujikaza.
408. Mwenye kuchinja hachelei kuchuna.
409. Mwenye kuumwa na nyoka akiona jani hushtuka.
410. Mwenye macho haambiwi tazama.
411. Mwenye mdomo hapotei.
412. Mwenye nguvu mpishe.
413. Mwenye njaa hana miko.
414. Mwenye pupa hadiriki kula tamu.
415. Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
416. Mwenye shoka hakosi kuni.
417. Mwenye tumbo ni tumbole, angafunga mkaja.
418. Mwenzako akinyolewa wewe tia maji.
419. Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana.
420. Mwili wa mwenzio ni kando ya mwilio.
421. Mwizi hushikwa na mwizi mwenziwe.
422. Mwomba chumvi huombea chunguche.
423. Mwosha hadhuru maiti.
424. Mwosha huoshwa.
425. Mwosha husitiri maiti.
426. Mzaha,mzaha, mara hutumbuka usaha.
427. Mzazi haachi ujusi.
428. Mzigo usiouweza unaubebea nini?
429. Mzigo Wa mwenzio ni kanda Ia usufi.
430. Mzika pembe ndiye mzua pembe.
431. Mzowea kutwaa, kutoa ni vita.
432. Mzowea vya kunyonga, vya kuchinja haviwezi.
433. Mzungu Wa kula hafundishwi mwana.
434. Nahodha wengi, chombo huenda mrama.
435. Nani kama mama?
436. Natuone ndipo twambe, kusikia Si kuona.
437. Nazi haishindani na jiwe.
438. Nazi mbovu harabu ya nzima.
439. Ndege mjanja hunaswa na tundu bovu.
440. Ndege mwigo hana mazowea.
441. Ndevu sio shani, hata beberu anazo.
442. Ndugu chungu, jirani mkungu.
443. Ndugu mwui afadhali kuwa naye.
444. Ndugu wakigombana, chukua jembe ukalime, wakipatana chukua kikapu ukavune.
445. Ngoja! ngoja? huumiza matumbo.
446. Ngoma ivumayo haidumu.
447. Ngoma ivumayo haikawii kupasuka.
448. Ngoma ya kitoto, haikeshi.
449. Ng'ombe avunjikapo guu hurejea zizini.
450. Ng'ombe haelemewi na nunduye.
451. Ngombe wa Maskini hazai.
452. Ngozi ivute ili maji. ( Udongo upate uli maji )
453. Nguo ya kuazima, Haistiri matako.
454. Nia njema ni tabibu, nia mbaya huharibu.
455. Nifae na mvua nikufae na jua.
456. Nimekula asali udogoni, utamu ungali gegoni.
457. Nimekupaka wanja, wewe wanipaka pilipili.
458. Nimerejesha kikombe na kisahani chake.
459. Njia ya muongo fupi.
460. Njia ya mwongo ni fupi.
461. Njia ya siku zote haina alama.
462. Nta Si asali; nalikuwa nazo Si uchunga.
463. Nyani haoni kundule, huliona la mwenziwe.
464. Nyani haoni kundule.
465. Nyimbo mbaya haibembelezewi mtoto.
466. Nyimbo ya kufunzwa haikeshi ngoma.
467. Nyongeza huenda kwenye chungu.
468. Nyota njema huonekana asubuhi.
469. Nyumba usiyolala ndani huijui ila yake.
470. Nyumba ya udongo haihimili vishindo.
471. Nzi kufa juu ya kidonda Si haramu. (Jihadi ya nzi, kufa kidondani)
472. Ondoa dari uwezeke paa.
473. Pabaya pako Si pema pa mwenzako.
474. Padogo pako Si pakubwa pa mwenzako.
475. Painamapo ndipo painukapo.
476. Paka akiondoka, panya hutawala.
477. Paka hakubali kulala chali.
478. Paka hashibi kwa wali, matilabaye ni panya.
479. Paka wa nyumba haingwa.
480. Panapo wengi hapaharibiki neno.
481. Papo kwa papo kamba hukata jiwe.
482. Pele hupewa msi kucha.
483. Pema usijapo pema; ukipema Si pema tena.
484. Penye kuku wengi usimwage mtama.
485. Penye mafundi, hapakosi wanafunzi.
486. Penye mbaya wako, hapakosi mwema wako/na mwema wako hakosi.
487. Penye miti hakuna wajenzi.
488. Penye nia pana njia.
489. Penye urembo ndipo penye urimbo.
490. Penye wazee haliharibiki neno.
491. Penye wengi pana mengi.
492. Penye wengi pana Mungu.
493. Pilipili usoila, wewe inakuwashia nini?
494. Pole pole ndio mwendo.
495. Pwagu hupata pwaguzi.
496. Radhi ni bora kuliko mali .
497. Radhi za wazee, ni fimbo.
498. Sahani iliyofunikwa, kilichomo kimesitirika.
499. Sahau ni dawa ya Waja.
500. Samaki mmoja akioza, huoza wote.
501. Samaki mpinde angali mbichi.
502. Shida haina hodi.
503. Shida huzaa maarifa.
504. Shika! Shika! na mwenyewe uwe nyuma.
505. Shimo Ia ulimi mkono haufutiki.
506. Shoka lisilo mpini halichanji kuni.
507. Si kila king'aacho ni dhahabu.
508. Si kila mwenye makucha huwa simba.
509. Si Mungu mtupu na mkono wa mtu.
510. Sikio halilali na njaa.
511. Sikio halipwani kichwa. (Sikio halipiti kichwa).
512. Sikio Ia kufa halisikii dawa.
513. Siri ya mtungi aijuaye ni kata.
514. Sitaacha kula mkate kwa kuogopa kiungulia.
515. Siku njema huonekana asubuhi.
516. Siku utakayokwenda uchi, ndiyo siku utakayokutana na mkweo.
517. Siku ya kufa nyani, miti yote huteleza.
518. Siku za mwizi, arubaini.
519. Simba mwenda kimya (pole) ndiye mla nyama.
520. Simbiko haisimbuki ila kwa msukosuko.
521. Sio shehe bali ni shehena.
522. Siri ya maiti aijuaye muosha.
523. Sitafuga ndwele na waganga tele.
524. Sitapiki nyongo harudi haramba.
525. Subira ni ufunguo Wa faraja.
526. Sumu mpe paka, mbuzi utamdhulumu.
527. Sumu ya neno ni neno.
528. Tabia ni ngozi ya mwili.
529. Tamaa mbele, mauti nyuma.
530. Taratibu ndio mwendo.
531. Tawi kavu kuanguka si ajabu.
532. Teke Ia kuku halimuumizi mwanawe
533. Tonga si tuwi
534. Tunda jema halikawii mtini.
535. Ucheshi wa mtoto ni anga Ia nyumba.
536. Ujuzi hauzeeki.
537. Uchungu wa mwana, aujue mzazi.
538. Udongo uwahi ungali maji (Udongo upate uli maji)
539. Udugu wa nazi hukutania chunguni (Udugu wa nazi hukutana pakachani)
540. Uji hajauonja, tayari ushamuunguza
541. Ukenda kwa wenye chongo, fumba lako jicho.
542. Ukimpa shubiri huchukua pima.
543. Ukimuiga tembo kunya, utapasuka Makalio.
544. Ukimwamsha alolala utalala weye.
545. Ukinyofoa mnofu, ukumbuke kuguguna mfupa.
546. Ukiona kwako kunaungua kwa mwenzako kunateketea.
547. Ukiona moshi, chini kuna moto.
548. Ukiona neno, usiposema neno, hutapatikana na neno.
549. Ukiona vinaelea, vimeundwa.
550. Ukiona zinduna, na ambari iko nyuma.
551. Ukistahi mke ndugu, huzai nae.
552. Ukitaja nyoka, shika fimbo mkononi.
553. Ukitaka kula nguruwe, chagua aliye nona.
554. Ukitaka salama ya dunia, zuia ulimi wako.
555. Ukiujua wa mbele, nina ujua wa nyuma.
556. Ukupigao ndio ukufunzao.
557. Ukuukuu wa kamba Si upya wa ukambaa.
558. Ulimi hauna mfupa.
559. Ulimi unauma kuliko meno.
560. Ulipendalo hupati, hupata ujaaliwalo.
561. Ulivyoligema, utalinywa.
562. Umeadimika kama la jogoo.
563. Umegeuka mung'unye waharibika ukubwani.
564. Umejigeuza pweza, unajipalia makaa?
565. Umekuwa bata akili kwa watoto?
566. Umekuwa nguva, huhimili kishindo?
567. Umeruka mkojo unakanyaga mavi.
568. Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
569. Unajenga kwa mwenzio na kwako kunaporomoka!!
570. Unakuja juu kama moto wa kifuu.
571. Unamlaumu mwewe, kipanga yuwesha kuku.
572. Ungalijua alacho nyuki, usingalionja asali.
573. Ushikwapo shikamana (Ukibebwa usijiachie).
574. Usiache kunanua kwa kutega.
575. Usiache mbachao kwa msala upitao.
576. Usiache tawi kabla ya kushika tawi.
577. Usiandikie mate na wino ungalipo
578. Usicheze na simba, ukamtia mkono kinywani.
579. Usijifanye kuku mweupe.
580. Usikaange mbuyu ukawaachia wenye meno
581. Usile na kipofu ukamgusa rnkono.
582. Usimgombe mkwezi, nazi imeliwa na mwezi.
583. Usiniache njia panda.
584. Usinikumbushe kilio matangani.
585. Usinipake mafuta kwa nyuma ya chupa.
586. Usinivishe kilemba cha ukoka.
587. Usione simba kapigwa na mvua.
588. Usipoziba ufa utajenga ukuta.
589. Usisafirie nyota ya mwenzio.
590. Usisahau ubaharia kwa sababu ya unahodha.
591. Usishindane na Kari; Kari ni mja wa Mungu.
592. Usitukane wagema na ulevi ungalipo.
593. Usitukane wakunga na uzazi 'ungalipo.
594. Utakosa mtoto na maji ya moto.
595. Usiyavuke maji usiyoweza kuyaoga.
596. Utaula na chua kwa uvivu wa kuchagua.
597. Vita havina macho.
598. Vita si lele mama.
599. Vita vya panzi, neema ya kunguru
600. Waarabu wa pemba, hujuana kwa vilemba
601. Wache waseme.
602. Wafadhilaka wapundaka.
603. Wagombanao ndio wapatanao.
604. Watu wanahisabu nazi, wewe unahisabu makoroma.
605. Wapiganapo tembo wawili ziumiazo ni nyasi.
606. Watetea ndizi, mgomba si wao.
607. Wazuri haweshi.
608. Wema hauozi..
609. wengi wape.
610. Zinguo la mtukufu, ni ufito.
Kamusi ni hazina la lugha
METHALI, NAHAU NI VIPERA VYA SEMI.
                (Fasihi Simulizi)
Fasihi simulizi ina tanzu zake na Semi ni moja ya tanzu zake. Utanzu huu nao una VIPERA vyake ambayo ni methali, nahau, misemo, simo, vitanza ndimi, vichezea meno na mgafumbo ambayo hujumuisha vitendawili, chemsha bongo, malumbo na mizungu.

Katika somo hili nitaelezea kwa kifupi maana na kutoa mifano ya Methali na Nahau na kuonesha ukaribu wa nahau, misemo na methali.

Methali na nahau zote ni
 semi zitumiazo lugha fupi fupi na ya mkato.

Methali
Maana.
Methali ni usemi wa kimapokeo, japo zipo methali zinazozaliwa kila wakati na nyingine kufa. ambao unaotumiwa kwa kufumbia jambo kwa maneno ya kawaida bali kwa njia ya mkato huku ukibainisha ukweli au kutolea ushauri kwa kulenga kwa usahihi kile kinachozungumziwa.

Kwa ufupi methali ni kauli inayobeba busara au falsafa za jamii husika.

Mifano ya methali za kimapokeo ni:
i. Pema usijapo pema ukipema si pema tena.
ii. Kozi mwana mandanda kulala njaa kupenda.
iii. Mwenda omo na tezi marejeo ni ngamani.
iv. Mwapiza la nje hupata la ndani.
v. Macho hayana pazia.
vi. Ukilima pakubwa ukivuna pamekwisha.

Mifano ya methali zilizozaliwa hivi karibuni kwa uchache ni:
i. Usiteme 'big G' yako kwa karanga za kuonjeshwa.
ii.Ukilima shamba njiani ujue kulinda ndege.
iii.Ukitaka kujua mwenendo wa mjinga mvishe kilemba.
iv. Kiyoo cha gari hakifungwi katika tairi ya gari
v. Ama kweli kama hujui unakokwenda huwezi kupotea.
 vi. Akimbiaye peke yake siku zote yeye ni mshindi.
vii. Usiku rafikiye ni giza.l

Misemo
Maana
Msemo ni fungu la maneno lenye maana mahsusi lenye  kutoa fundisho ama kuelezea dhana fulani kwa j amii lisilo na kitenzi ndani yake.

Wengi huchanganya misemo na nahau. Tofauti kubwa kati ya tungo hizi ni kitenzi. Nahau huwa na kitenzi lakini msemo hauna kitenzi ndani yake

Ifuatayo ni mifano michache ya misemo ya Kiswahili na maana zake:
i. Mkono wa birika=mchoyo
ii. Sindano na uzi. =ushirikiano au umoja
iii. Kiti moto=nyama ya nguruwe  au misukosuko ya madaraka.
iv. Hamadi kibindoni=akiba uliyo nayo mkononi.
v. Mwana haramu= mtoto wa nje ya ndoa.
vi. Kiwi cha macho= tamaa ya mapenzi.
viii. Mkono mrefu = mwizi
viii. Akali ya watu= watu wachache.
ix. Umti wa watu = watu wengi.

Katika mkutadha wa maongezi aghalabu misemo huongezewa kitenzi na kutenda kazi ya nahau lakini maana hubakia kuwa ile ile ya awali.

Nahau
Maana
Usemi mfupi ulio na kitenzi unaotumia maneno ya kikawaida, lakini yakiwa na maana iliyojificha na iliyotofauti na maana ya maneno hayo.
mfano:
i). Kujikaza kisabuni = kutia bidii,
ii).kuvaa miwani = kulewa,
iii).Kuoga mwaka= kusherehekea kumaliza mwaka kwa salama.

 Zifuatazo ni nahau maarufu za lugha ya Kiswahili. Kila lugha ina nahau zake na kusudio kuu la matumizi ya nahau  ni kuifanya lugha kuwa safi.Neno hili lina asili ya Kiarabu na maana yake ya asili ikiwa ni usafi wa lugha ikimaanisha matumizi sahihi ya lugha.

1 Amekula chumvi nyingi=ameishi miaka.
    mingi
2, Ana mkono wa birika= mtu mchoyo
3.Ametutupa mkono= amefariki, amekufa
4.Ameaga dunia=amekufa, amefariki
5.Amevaa miwani=amelewa
6.Amepiga kite=amependeza
7.Amepara jiko=kaoa
8.Amefumga pingu za maisha=ameolewa
9.Anawalanda wazazi wake =
    kawafanana wazazi wake kwa sura
10. Kawachukua wazazi wake=anafanana
       na wazazi wake kwa sura na tabia.
11.Kawabeba wazazi wake = anawajali na
      kuwatunza wazazi wake.
12. Chemsha bongo = fikiri kwa makini na
       haraka.
13.Amekuwa toinyo=hana pua.
14. Amekuwa popo =amekuwa kigeugeu
15. Ahadi ni deni = timiza ahadi yako
16.Amewachukua wazee wake =
      anawatunza vizuri wazazi
17.Amekuwa mwalimu= yu msemaji sana
18.Amemwaga unga = amefukuzwa kazi
19..Ana ulimu wa upanga=ana maneno
     makali
20.Ameongeza unga = mepanda cheo
21.Agizia risasi = piga risasi
22.Kuchungulia kaburi= kunusurika kifo
23..Fyata mkia= nyamaza kimya
24.Fimbo zimemwota mgongoni=ana
     alama za mapigo ya fmbo mgongoni
25.Hamadi kibindoni= akiba iliyopo
      mkononi]
26.Hawapikiki chungu
       kimoja=hawapatani kamwe
27.Kupika majungu = kumteta mtu kwa
       siri
28.Kumvika mtu kilemba cha ukoka =
      umsifu mtu kwa unafiki
29Kula mlungula /kula rushwa = kupokea
      rushwa
30.Kupelekwa miyomboni = kutiwa au
      kupelekwa jandoni
31.Kujipalia mkaa =  ujitia matatani
32.Kumeza au kumezzea mate = utamani
33.Kumuuma mtu sikio = kumnong'oneza
      mtu jambo la siri
34.Kumpa nyama ya ulimi =
     kumdanganya mtu kwa maneno
     matamu
35.Kumchimba mtu  = kumpeleleza mtu
      siri yake
36.Kutia chumvi  katika mazungumzo  =
      uongea habari za uwongo
37.Vunjika moyo = kata tamaa
38.Kata maini = kutia uchungu
39. Kujikosoa = kujisahihisha
40.Kutia utambi  = kuchochea ugomvi
41.Kumeza maneno  = kutunza siri
      moyoni
42.Kula njama kufanya mkutano wa siri.
43.Kumkalia mtu kitako = kumsema
       au kumsengenya mtu
44.Kupiga mtu vijembe = kumsema mtu
      kwa fumbo
45.Kiinua mgong = malipo ya pongezi ya
      uzeeni bada ya kustaafu kazi
46.Kazi ya majungu = kazi ya kumpatia
      mtu posho
47.Kaza kamba au kaza roho =usikate tamaa
48..Kumwonyesha mgongo = kujificha
49.Kuona cha mtema kuni = kupata
      mateso au kuuliwa kwa kukatwa
      kichwa
50.Maneno ya uwani = maneno yasiyo na
      maana au porojo
51.Mate ya fisi = tamaa kupita kiasi
52.Kata tamaa = vunjika moyo kutokuwa
      na hamu ya jambo fulani.
53. Mbiu ya mgambo = tangazo
54.Mungu amemnyooshea kidole = mungu amemuadhibu
55.Mkubwa jalala = kila  lawama hutupwa kwa mkubwa
56.Mkaa jikoni= mvivu wa kutembea
57.Mungu si Athumani= mungu hapendelei
58.Paka mafuta kwa mgongo wa chupa = danganya
59.Usiwe kabaila  = usichume tokana na jasho la mwingine
60.Usiwe kupe = fanya kazi
61.Usiwe bwanyenye = usichume kwa vitega uchumi vyake.
62. Usiwe na mirija = usinyonye wenzako
63.Utawala msonga= utawala wa wachache
64.Usiwe nyang'au = nchi moja kuifanyia nyingine  ubaya na udhulumati.
65.Usiwe kikaragosi = nchi kuwa kibaraka wa nchi kubwa.
66.Usiwe chui katika ngozi ya kondoo=kujifanya rafiki kumbe ni adui
67.Kutoa ya mwaka =kufanya jambo zuri na la pekee
68.Kumpa mtu ukweli wake = kumwambia mtu wazi ubaya wake.
69.Pua kukaribiana kushikana na uso =kukunja uso kwa hasira
70.Kusema kutoka moyono=kunena kilicho kweli
71.Sina hali= sijiwezi kiuchumi
72.Kupiga uvuvi = kukaa tu bila kazi
73.Kupiga kubwa = kwenda moja kwa moja, kusepa
74.Kumwekea mtu deko = kulipiza  kisasi
Mtu mwenye ndimi mbili = kigeugeu
75.Miamba ya mitishamba =wanga hodari wa kienyeji
76.Kupiga supu = kutegea kazi wengine wafanye
77.Kupiga mali shoka = kugawana  mali au urithi
78. Kula vumbi kuhangaika maisha,  pata tabu kutafuta riziki
79.Mafungulia ng'ombe =muda wa kati ya saa mbili na saa tatu asubuhi.
80.Kutia kiraka =fichia siri
81.Kumlainisha mtu= kumzungumzia mtu maneno matamu mpaka akubali matakwa yako.
82. Kupiga pamba=kuvaa vizuri
83.Kufulia = kuishiwa
84.Umangimeza=uongozi wa kuamrisha watu, udikiteta au uongozi wa imla

Na hizi ni kwa uchache tu, ziko nyingi za zamani na za sasa ambazo sijazielezea kama: kupiga kite, kuondoa kiwi cha macho, kupiga hema, kunawa mikono, nakadhalika.
TIME ya Januari 12, 2004 
Ugonjwa wa sukari umekuwa tishio siku hizi. Ugonjwa huu haushambulii wazee, watoto au vijana tu  bali makundi yote haya yamekuwa yakisumbuliwa na ugomjwa huu.


Tishio hili haliko Tanzania peke yake bali liko ulimwenguni kote Hata hivyo viwango vya kuathirika huweza kutofautiana toka nchi moja na nyingine lakini haipo nchi iwezayo kudai iko salama na tishio la ugonjwa huu.

Ugonjwa huu hauna tiba ila zipo dawa za kumfanya mgonjwa kuishi kwa matumaini na kupunguza athari zitokanazo na ugonjwa huu.

Pamoja na dawa hizi wagonjwa wengi tunashindwa kufuata masharti ya kudhibiti kikamilifu athari zitokanazo na ugonjwa huu katika miili yetu.

HII NI KUTOKANA NA KUTOJUA ATHARI za ugonjwa huu kwetu  PILI KUTOJUA NJIA SAHIHI ZA KUDHIBITI ATHARI HIZI.

Sasa hivi wagonjwa wa sukari tunadanganywa sana na watu kuhusu tiba na kupoteza maelfu ya pesa pasipo na mafanikio.Njia sahihi ni kutumia dawa za hospitali za kuzuia  athari zitokanazo na   ugonjwa huu toka kwa waganga wa mahospitali. Tiba mbadala sahihi  haswa haswa ni vyakula na mazoezi kusaidia hizi  hizi za mahospbinitalini katika kudhibiti athari zitokanazo na ugonjwa huu.

Dawa za hospitalini ziko katika makundi makuu matano.
1.Kwanza zipo za kuchochea kongosho kuzalisha isulin zaidi (Sulfonylureas).
2. Pili ni (Meglitinides) hizi nazo kama kundi la kwanza huishajiisha kongosho kuzalisha insulin
    zaidi
3.Kundi la tatu ni (Biguanides) Hizi hulikataza ini kutoa sukari (glucose) nyingi na husisimua misuli
   kutumia sukari zaidi kutoka katika damu.
4.Kundi la nne linaitwa (Thiazolidinediones) Hizi ni dawa za hivi karibuni tu ambazo huiwezesha
   insulin kusukuma (gulucose) sukari na mafuta kuingia katika misuli kwenda kuzalisha nishati
   mwilini.
5.Kundi la tano ni (Alpha -Glucosidase Inhibitors) hii hufannyia kazi kwenye utumbo mwembamba
   kuzuia mikate na vyakula vya wanga  kubadilishwa kuwa sukari (glucose)

Pili ni vema kujipima kiasi chako cha sukari katika damu  ili kujua kupanda na kushuka kwa sukari katika mwili wako.

Dalili ziashiriazo kuwa na ugonjwa huu za awali ni hizi:
1.Kukojoa mara kwa mara  hasa usiku.
2.Kuona kwa mawengewenge, Macho kupoteza uoni wake wa kawaida.
3.Kuwa na kiu kali isiyoisha.
4.Kuwa na njaa kali kama ya mtoto.
5.Kupoteza uzito kusiko kwa kawaida kwa kipindi kifupi.
6.Kuwa na vidonda visivyopona haraka.
7.Mwili kuchoka kwa hali isiyo ya kawaida.
8.Kupoteza hamu ya tendo la ndoa.
9.Kiuno kuuma hasa ukitaka kusimama.
10.Miguu na mikono kufa ganzi hasa nyakati za asubuhi.
11.Kutopata usingizi mapema na ukilala hutaki kuamka na uamkapo unakuwa umechoka sana.
12.Kupata choo kigumu na huwa hakipatikani kwa wakati wa kawaida.
13.Uzito wa mwili kuongezeka sana na huku huli sana.

Dalili  za ugonjwa huu ni nyingi mno ila za msingi ni hizi hapo juu.Tukiwa wagonjwa wa sukari tunapaswa kushirikiana na kubadilishana uzoefu na njia za kudhibiti athari zake.Hili hakika ni muhimu kulipata kutoka kwa kila mmoja wetu.KUMBUKA UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHDIFU.

Niligundua nina ugonjwa huu toka mwaka 1997 lakini sikuwa na dalili nilizoeleza hapo juu.Tatizo la awali kwangu lilikuwa kuongezeka uzito na kuvimba miguu.Hali hii iliniogopesha nikajihisi  nina tatizo la moyo au figo hivyo nikawaona madakitari na ndipo nilipobainika kuwa nina ugonjwa wa kisukari.

Nilianza kusoma maandiko mbalimbali ya ugonjwa huu na ndipo  nilipo kutana na gazeti la TIME la Januari 12, 2004  gazeti hili lilieleza kwa kina juu ya ugonjwa huu. Waandishi wa makala haya ni Christine Gorman na Kate Noble..Makala yao yalikuwa na kichwa kilichosema "  Why so many are gating Diabetes" Ikiwa na maana KWANINI   KISUKARI KINAWAKUMBA WENGI. Lilikuwa ni swali lilotaka majibu.Humo walieleza kuwa kisuksri hakijapatiwa dawa  kamili na haijulikani kwa hakika  kwanini watu wanakiugua.

Maelezo ya tafiti mbali mbali yalionesha nini chanzo yalitolewa na nini kifanyike kuzuia kupata ugonjwa huu  yalitolewa pia.

Mtindo wa maisha , mazingira  na urithi vilielezwa kuwa ni sababu kubwa za mtu kupata ugonjwa huu.Kwa kawaida kisukari si ugonjwa wa kuambukiza.Ni ugonjwa  ambao mwili unashindwa kutumia sukari kama inavyotakiwa.

Kisukari ni ugonjwa  ambao unaweza  kutambulika kwa namna kuu nne.
1. Kwanza ni kwa njia ya kuangalia kiwango cha sukari  katika damu.Kiwango  sahihi  kisizidi
    m/moll 7  kabla ya kula chochote ndani ya saa 8 hadi 10, Kitaalamu upimaji huu huitwa  FBG
  (Fasting Blood Suger).Kwa kawaida mwili  ukiwa hauna tatizo katika kutumia sukari baada ya
   muda huo lazima sukari katika damu iwe katika kiwango sahihi.Sukari ikiwa zaidi  ya kiwango
   hicho lazima mwili una shida katika kubadili sukari katika damu kuwa nishati.

2. Kipimo cha pili cha kujua mtu ana sukari  au hana ni  (GTT) Glucose Tolerance Test. Kikawaida
    m/moll za mtu asiye na kisukari ni chini ya 7.  Kipimo hiki ni baada ya kula na kutumia sukari,
    Kama baada ya kula na kutumia sukari  kiwango cha sukari katika damu kitaonekana kuwa sukari
    katika damu ni kati ya 7 na 11 m/moll muhusika  atakuwa si mwenye kisukari.

3. Namna ya tatu ya kujua kuwa mtu ana sukari ni kwa njia ya kuona  jinsi 'insulin' inavyogoma
    kufungua 'cell' ili ipokee sukari kutoka katika damu  ikazalishe nishati. Insulin ni homoni
    izalishwayo na kongosho ifanyayo kazi  kama ufunguo wa kufungua mlango.Yaweza ikawa nyingi
    na ya kutosha lakini ikagoma kufungua au ikawa kidogo ikawa haitoshi.Wenye uhaba wa insulini
    mara nyingi ni wale wa aina ya kwanza ya kisukari na wenye nyingi  iliyogoma ni wale wa aina ya
   pili ya kisukari.Kipimo hiki ni kigumu kidogo  katika kupima kisukari kwani  sukari ya mgonjwa
   yaweza kuwa sawa lakini insulini haipo kabisa  ama ipo lakini imegoma kufanya kazi.Kipimo hiki
   kinaitwa (IR) Insulin Resistance.

4 .Namna ya nne ni kuisha kwa sukari mwilini. Hali hii inaitwa (hypoglysomia) Sukari mwilini ikiwa
    chini ya ' mill moll' nne (4) ni hatari hivyo inatakiwa kupandishwa haraka kwa kumpatia mgonjwa
    kitu cha sukari haraka ili kuipandisha.Wagonjwa wengi wa sukari hupoteza maisha sukari yao
    ikishuka sana zaidi ya hapo.

Namna ya kudhibiti ongezeko la sukari ni KUACHA mazoea mabaya ya kunywa pombe kali na za kupitiliza, kula nyama choma kwa wingi, kula chips mayai, kunywa soda sana, kuvuta sigara, kula vyakula viyeyushwavyo haraka tumboni, kutofanya mazoezi na kutunza unene, Ndiyo, wapo wembamba na wana kisukari lakini hatari kubwa ya kupata kisukari iko kwa watu wanene zaidi.



Pata maelezo zaidi toka katika clip yangu hii fupi ya dakika saba tu na naomba maoni  yako




Image may contain: 1 person, outdoor

BABU HASSANI SHAGHIRA MTHOO
Eliamini Hassan ALI Salimu Ali Msangi. 
Pata mtiririko wa ukoo wa Salimu Shaghira kutoka kwa BANGALALA kwa Ufupi.
Wasangi ni uzao wa Bangalala aliyetoka huko Kenya sehemu itwayo Usangi miaka mingi iliyopita.Bangalala alizaa watoto wawili Yambii na Mnyatta.
Mnyatta yeye alirudi Kenya.Kwa hiyo habari zake hazijulikani kwa upana.
Yambii akamzaa Mang'a.Mang'a naye akamzaa Ndorokwa.
Ndorokwa akazaa mtoto akamwita jina la baba yake Mang'a. Huyu Mang'a Jr. akamzaa Mahu.
Mahu akamzaa Akavyo..Akavyo akamzaa Kiyanga.
Kiyanga akamzaa Mfuta, Mfuta akazaa watoto wawili Nzano na Setonga.
Sasa hivi nafuatilia uzao wa Setonga.
Yeyote anayejua uzao tokea setonga hadi hapi alipo anipe mtiririko huo.
Wasangi kwa sasa tiko wengi ili uweze kutambulika kuwa wewe ni nani na ni wa baba au ni wa kutoka kwa babuci yupi tunapaswa tuandike majina matatu au zaidi.Jina moja lilkifuatwa na Msang kwa mfano Abdalla Msangi, Ramadhani Msangi, au Adam Msangi halitoshi kukutambulisha kikamilifu.
Sasa, baada ya hilo angalizo, tuendelee na uzao wa Nzano.
Kwa upande wa Nzano yeye alioa wanawake wengi. Kwa jinsi hii akazaa watoto wanne. Ijumbi akiwa ni mtoto wake wa kwanza akifuata Kisarika na Komeja.
Mroki alikuwa mtoto wa nne wa Nzano, na wa mwisho kwa mke wa mwisho.
Ijumbi alizaa ukoo wa kina Senakanga ambao ni kina. Senguji na Bondera.
Komeja akawazaa Mlawa, Mramba, Idhina na Mchaimwa Huyu Mchaimwa alikuwa mwanamke uzao wake ni ukoo wa Saidi Mcholo.
Kisarika akawazaa Kisineni, Nguma,Ishiwa, Mghamba na Kinyonge Kinyonge ukoo wake ni wa kina Chakupewa.
Kisarika, Kisineni, Nguma, Mghamba koo zao ni za kufuatilia sina maeleza yake.
Tukija kwa Mroki mtoto wa Nzano wa mwisho kwa mke mdogo, huyu Mroki alimzaa mtoto mmoja akamwita Mthoo. Mthoo alizaliwa peke yake kama alivyozaliwa baba yake.
Mthoo alizaa watoto watatu Shaghira,Vichike na Nguluma.Vichike alikwa ni mwanamke na alikuwa ndiye mtoto wa kwanza kuzaliwa, akifuatiwa na Shaghira na Nguluma akiwa ni mziwanda.
Shaghira alikuwa mwiisilamu na aliitwa(Ali). Shaghira alizaa watoto wanne Hassaniakiwa wa kwanza akifuatiwa na Salimu, Ibrahimu na Selemani akiwa ndiye wa mwisho kwao.
Salimu akawazaa Ali (Shaghira Jr), Hatibu na Nauche. Huyu ni Nauche ni wa kike na ni kitinda mimba wa babu Salimu aka Kigingi
(Mbishi yakwe Namwai)
Chui aliyezaliwa na Namwai. Namwai ni mama yake.Babu Salimu.Babu Salimu alikuwa akijigamba kwa namna hiyo.
Mimi nimezaliwa na Ali (Shaghira Jr.) Salimu mtoto wa kwanza wa Salimu. Niliitwa Hassani jina la baba mkubwa wa babangu .hivyo mimi ni Hassan Jr
Huyu Hassan ambaye nimeitwa jina lake anaitwa Mthoo jina la babu yake hivyo na mimi ninatwa Mthoo wa tatu. Jina lake jingine la utani (nick name) aliitwa TILISHO.
Na mimi nina watoto Watatu Ali, Riziwani na Hatibu.
Ali ni jina la baba wa babu zangu. Alikuwa kasilimu na alikuwa imamu.
ALI mwanangu ni Ali wa tatu.
HUU NDIO MTI WA UKOO wa Salimu Ali (Shaghira)Mthoo.
KOO NYINGINE HAPO KATIKATI NI ZA KUJAZIA.
SIMULIZI hii nimesimuliwa na Babu Hassan ALi ambaye kwa jina la babu aliitwa Mthoo. Na mimi pia ni Mthoo wa tatu.
Eliamini : Msangi Nawashukuruni nyote mlio like post hii. Kwa kuwa tawi letu limeanzia kwa Nzano, nitaendeleza mtambao wa Wasangi wa tawi hili.Naomba ushirikiano wenu Wasangi wa kwa Nzano na Setonga.
Like · Reply · 1 h
Malaho Omari :Hahahaha weee kaka umenifurahisha sana mimi ni malaho mtoto wa mzee OMARI (SABUNI) wewe tumeachana hapo kwa setonga setonga alimzaa marisa na shanjarika marisa akamzaa Malaho na huyu malaho akamzaa salimu malaho JUMA malaho (babake mshare) Omari malaho...See more
Like · Reply · 1 hr
Eliamini Msangi :VYAKWA KIAMBO TUKO KARIBU SANA NAO, NAMI NITAFUATILIA.wasangi bwana wameenea sana.Omari mshare yule aliyekuwa akiishi Kwakoa.Mzee BONDERA baba yake na JUMANNE NA ERNEST BONDERA.
Chini kushoto ni babu Hassan Ali kulia babu Salimu Ali
Matokeo kidato cha nne mwaka 2016

http://necta.go.tz/matokeo/2016/ftna/index.h

*MATOKEO YA KIDATO CHA NNE YATOKA*

Baraza la Mitihani nchini(NECTA) latangaza matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2016.
Wavulana wafaulu kwa 73.26% na Wasichana 67%.

*MATOKEO YA KIDATO CHA NNE YATOKA*

Baraza la Mitihani nchini(NECTA) latangaza matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2016. Wavulana wafaulu kwa 73.26% na Wasichana 67%. Soma

Kujua Shulekidato kumi Bora na kumi za Mwisho bofya link ifuatayo


https://goo.gl/NZWTeW


Nimepoteza   funguo za pikipiki yangu na 'remorte' yake na barua (documents) za kikazi maeneo ya Mkuyuni jijini Mwanza.Yeyote aliyeviokota namwomba anirejeshee. Kunazawadi nzuri. Nipigie kwa Namba+255754366352huu.upotevu umetokea Jumatano ya tarehe. 18-01-2017

Maeneo nilikopita hiyo juzi. Niliipaki pikipiki kwa fundi kwa marekebisho madogo Mkuyuni  Nilichua ufunguo nikapakia daladala   kwenda mijini kwani nilikuwa napeleka form zaHBngu za kustaafu ofisi za PSPF.Nilipotoka PSPF  nilienda Jiji Mwanza kwa kupeleka nakala ya form za form za PSPF nikiwa ofisi za TSD jiji, ndipo nilipobaini upotevu wa funguo  hizo. Nilifuatilia ofisi za PSPF bila mafanikio.Nikafuatilia nilikoacha pikipiki huenda sikuzichomoa nako sikufanikiwa.Nikaamua kubadili 'switch'.

Nikiwa katika harakati za kubadili hiyo 'switch'  nikapigiwa simu kuwa nilipotoa form za PSPF nilisahau juu ya dirisha 'Salary slips' ambazo jioni yake Ida Mangasa jirani yangu aliniletea.

Kasheshe ni hizo nyaraka zangu za kikazi na ufunguo wa 'tank' la mafuta na 'lock' ya pikipiki.

Hizo barua nilikuwa nazo nilipokuwa
nabadili 'switch' hapo Mkuyuni.

Tumaini langu ni kwa wewe mkazi wa Mwanza utakayeusoma ujumbe huu na ukawa umebahatika kuona au kusiki aliyeokota barua hizo au kuona funguo  hizo nisaidie kwa kunirejeshea vitu hivyo kwa kutumia namba ya simu nilotoa hapa ya +255754366352 au ya +255714366352.

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza