MBWA TISHIO KWA WAKAZI WA SWEYA A NA B AULIWA

Mtoto James Magoti  akisaidiwa 
na kaka yake kuonesha
 sehemu aliyoumwa
Watoto watano, mbuzi na mbwa wa Justine Mwenula wang’atwa katika mitaa ya Sweya A na B Nyegezi, viunga vya Jiji la Mwanza na mbwa anayeshukiwa kuwa na kichaa.

Mbwa huyu ameanza kung’ata kuanzia Jumamosi ya tarehe 24, Junuari watoto watatu, James Magoti, Irene Mashaka na aliyejulikana kwa jina moja la Bahati.

 Mbuzi aliyeng’twa ni wa ndugu John Ngugi na inasemekana aliuliwa hapo hapo na mbwa huyu.

Leo, Jumapili  tarehe 25 Januari, 2015, asubuhi, balozi Otieno Kadondi aongoza kundi kubwa la wana Sweya wakiwa wamebeba mikuki, nondo, marungu na magongo kumsaka mbwa huyu.

Mtoto Bahati na majeraha ya meno ya mbwa mgongoni.
Mwenyekiti mteule ndugu Joseph Masome naye hakuwa nyuma, alishiriki zoezi hili la kumsaka mbwa huyu aliyetokea kuwa tishio la mtaa wote wa Sweya ndani ya siku hizi mbili.

Hasira za wananch kwa mbwa huyu zilipanda zaidi pale mbwa huyu alipong’ata watoto wengine wawili mmoja mtoto wa Bahati ambaye ni bubu na mwingine ambaye jina lake halikupatikana kwa uhakika lakini ilidaiwa kuwa ni mjukuu wa Marehemu Chacha Kichele.

Baada ya msako mkali kuzunguka mitaa yote ya Sweya A na Sweya B wanakijiji walifanikiwa kumtia mikononi huyumbwa  na kumuua hapo hapo.

Katika harakati za kumsaka mbwa huyu mbwa wengi walionekana kuzagaa ovyo hapa na pale pasi na kufungiwa ndani kama inavyotakiwa kwa wanaofuga wanyama hawa.

Imefahamika pia kwamba kumezuka kamtindo ka baadhi ya watu kuwaingiza mbwa kwenye gari na kwenda kuwatupa sehemu za mbali hususani nje ya mji kwa dhana kuwa hawawezi kujua njia ya kurudi walikokuwa awali..


Wana kijiji katika harakati za kumsaka mbwa nwenye kichaa 
Hali hii inaonesha kuwa mbwa wanafugwa kiholela na wengi wakiwa hawajachanjwa kuwakinga na ugonjwa wa kichaa cha mbwa (rabies).

Wakati wa zoezi la kumsaka mbwa huyu, wananchi walisikika wakiilalamikia idara ya mifugo, jijini Mwanza kwa kushindwa kwake, kutimiza wajibu wake wa kudhibiti ufugaji holela wa mbwa na kuhimiza uchanjaji wa mbwa kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa.

“Gharama ya kumchanja mtu akinga’twa na mbwa kumkinga na kichaa cha mbwa ni zaidi ya laki moja.’’Mmoja wa wasakaji wa mbwa huyu alisikika akisema.
Ukweli unabakia pale pale  kuwa gharama za kumhudumia mtu anapong’atwa ni kubwa zaidi ya hapo haswa ikizingatiwa kuwa jamaa na majirani huingiwa na hofu na kushindwa kufanya shughuli zao kama kawaida na  kwa kuwa kunakuwepo na upoteaji wa muda mwingi katika kushughulikia matibabu.

Tunaitaka mamlaka husika kudhibiti kuzagaa kwa  mbwa na paka kiholela, jijini humu hali ambayo hubainishwa kwa kugongwa gongwa mbwa na paka mara kwa mara mabarabarani.


Mbwa aliyeuliwa 
Pamoja na udhibiti huu ni vyema uchanjaji wa mbwa na paka ukawa unafanywa kila mwaka.

Zoezi hili si tu kwamba litaleta utulivu bali  bado litakuwa ni njia mojawapo ya kuongeza pato la jiji.

Tatizo hili laweza kuonekana ni la hapa Sweya lakini laweza kuwa ni kiashiria cha uwepo kwa tatizo hili sehemu nyingine.


Balozi OTIENO Kadondi  aliyehamasisha usakaji wa 
mbwa huyu aliyekuwa tishio la mitaa miwili ya SWEYA.
Mwisho wa yote mbwa huyu alifukiwa kwenye shimo refu walochimba wana mtaa na kumfukia.

Wasiwasi ukabakia kwa wale waloumwa na mbwa huyu  juu ya kupatiwa matibabu sahihi na pia  kuchunguza mwenendo wa mbwa walioumwa na huyu anayedhaniwa kuwa na kichaa.

'Wananzengo' wakishuhudia akifukiwa
aridhini mbwa aliyekuwa tishio kwao







1 comment:

  1. Ufugaji mbwa kiholela udhititiwa maana ni hatari kwa watu

    ReplyDelete

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza