INDIA YADAI KUGUNDUA DAWA YA KUTIBU UKIMWI.

Dr. Rashidullah Khan, Mwenyekiti wa Baraza Kuu
 la Madawa India (CCIM), New Delhi,  India,
 akimpatia Afisa Mkuu wa kampuni ya madawa ya
 HOOTONE Dr. Sayyed Habib KarimTuzo bora
ya kitaifa kwa ajili ya "Utafiti juu ya dawa ya
tiba ya VVU na UKMWI " katika mkutano mkuu
uliojumuisha wajumbe  wote wa 'India Tibbi Congress'
uliofanyika huko Mumbai Desemba  ya  21, 2013.
Ni muda wa zaidi ya miaka thelathini sasa toka ugonjwa wa Ukimwi utambulike na tafiti nyingi zimefanywa kutoka kona mbalimbali za dunia kuutafutia tiba na kinga pasipo na mafanikio ya kuridhisha.

 Pamoja na tafiti hizo shirika la afya duniani limekuwa likifuatilia kwa karibu jitihada  za tafiti hizi  na pengine kuzisimamia au kuzichangia.

Lakini hali inavyoonekana suala hili kwa upande mmoja limekuwa lina sura ya ushindani ndani yake wa nani awe wa kwanza kuwa kinara wa ugunduzi huu.

Mashirika mengi ya kitafiti ulimwenguni yamekuwa yakitoa taarifa za tafiti zao zikiwa bado hazijaiva..

Majaribio yakuthibitisha dawa na chanjo zilizogunduliwa yamefanywa mengi na matokeo yaliyopokelewa ni mengi lakini cha ajabu tunaambiwa chanjo wala tiba haiko karibu kupatikana.

Lakini matumaini hayapo kwani inadaiwa yanahitajika marekebisho ya mapungufu yanayojitokeza.

Sababu kuu ya kushindikana kupatikana dawa au chanjo ni madai kwamba kirusi cha UKIMWI si aina moja na pia hujibadili badili haraka kwa kujihami na dawa au chanjo zilizopatikana.

Kwa maelezo na majaribio ya Wahindi waliyoyaonesha huenda wakawa wamefuzu.kupata  Dawa yaUKIMWI. Shuhuda za wagonjwa waliopona zinatia matumaini.

Katika ripoti ya utafiti wa Dawa yao ya  Unani Anti-HIV Drug  katika kikao cha kimataifa huko TIANJIN, CHINA tarehe 1-3 Desemba  2006, RIPOTI yao inatia matumaini.

Cha kushangaza ni kwamba hivi ni kwa nini bado WHO iko kimya hadi sasa kwa taarifa nzuri na za kutia matumaini kama hizi.

Kingine cha ajabu zaidi  ni viongozi wa nchi zetu hizi zinzoendelea  na wenye nafasi za kifedha kuzidi kukimbilia India kwa matibabu, Au sababu za kumiminikia kwao huko ni kama zile za kwa babu wa Loliondo.

Kama nasi tungekuwa na  uwezo nadhani hospitali zetu zingefungwa maana wote tungeishia India kama tulivyojazana kwa babu wa Loliondo.

Waswahili wanasema lisemwalo lipo na kama halipo laja.Wahindi hawataishia kutuokoa kwa usafiri wa bajaji bali nadhani watakuja kuwa magwiji wa masuala ya tiba pia.


Kwa  uthibitisho zaidi juu ya uponyaji huu, huu hapa  ushuhuda wa mgonjwa wa ukimwi aliyepona kwa dawa hii.

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza