Ikulu Yaweka Hadharani Hati ya Makubaliano ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue.

Ikulu  yaweka hadharani hati ya makubaliano ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, iliyotiwa saini na waasisi, hayati Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume Aprili 22, 1964.

Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani KarumeAprili 22, 1964, 

wakiweka sahihi za makubaliano ya Nuungano waTanganika na Zanzibar


Sahihi za waasisi wa Muungano
, aliwaambia waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kwenye kikao hicho kilichofanyikia  Ikulu, jijini Dar es Salaam juzi  Jumatatu,14 Aprili 2014. kuwa serikali imesikitishwa sana na maneno yaliyongelewa kuwa Muungano ni batili kwa kuwa hauna hati ya makubaliano.






IFUATAYO NI  HOTUBA HIYO

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAMKO LA KATIBU MKUU KIONGOZI KWA VYOMBO VYA HABARI
KUHUSU HATI YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
IKULU, DAR ES SALAAM, TAREHE 14 APRILI, 2014
______________________________ ____________________
Siku 12 zijazo tutasherehekea miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kuzaliwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wamezaliwa watu ndani ya Muungano huu na wengine wana wajukuu.
Inasikitisha sana kuwa leo, miaka 50 baadaye ipo dhana potofu inayojengwa kuwa Muungano huu si halali kwa vile hakuna Hati ya Muungano (Articles of the Union).
Waasisi wa Taifa letu ambao tarehe 22 Aprili, 1964 kule Zanzibar walitia saini Hati hiyo, mbele ya mashuhuda, nao wameonekana kama walichokifanya kilikuwa kiini macho, na kwa hiyo kwamba waliongoza Taifa jipya la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa msingi wa kiini macho hicho kwa miaka yote hadi Mwenyezi Mungu alipowaita.
Mambo yote mawili yametusononesha sana sisi Serikalini, na bila shaka yamewasononesha wananchi wanaoipenda nchi yao, wanaowapenda Waasisi wa Taifa letu na kuuenzi Muungano wao.
Madai ya kuonyeshwa Hati ya Muungano yalianza siku nyingi lakini hatukuweza kuamini hali itafikiwa ilipofikia, ambapo wapo watu wanathubutu kudai na kuapa kuwa Hati hiyo haipo.
Ukweli ni kuwa hati hiyo ipo, ilikuwepo siku zote. Hata hivyo, lazima tukubaliane kuwa zipo Hati fulani ambazo ni kiini cha uwepo wetu kama Taifa huru, Jamhuri huru na Muungano huru, ambazo tunazihifadhi kama mboni ya jicho. Hati hizo ni pamoja na Hati ya Uhuru wa Tanganyika ya mwaka 1961, Hati ya Tanganyika kuwa Jamhuri mwaka 1962, na Hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ya mwaka 1964. Hati za aina hii zinahifadhiwa maeneo maalum ambayo ni salama ili zisipotee wala kuharibika. Kwa kawaida hatuzitoi, tunazifungua ili kuzihifadhi kwa namna yoyote ile.
Lakini sasa maneno yanakua mengi, tuhuma zimekuwa nyingi, dhihaka zimekuwa nyingi, kiasi cha wananchi kuanza kutiwa mashaka iwapo kweli Hati ya Muungano ipo au la.
Hivyo, kwa maagizo na ridhaa ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninaleta mbele yenu Hati ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyotiwa saini Zanzibar na waasisi wetu, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Mzee Abeid Aman Karume, ili muione na kuwahakikishia Watanzania kuwa yanayosemwa kuwa hakuna Hati hiyo si kweli. Hati hiyo ipo tangu wakati huo, imetunzwa vizuri na waliotutangulia, tumeirithi, na tutaendelea kuihifadhi.
Na, tukiombwa kufanya hivyo na Mwenyekiti wa Bunge Maalum nina uhakika Rais ataridhia ipelekwe huko ili kuondoa mjadala wa kama Hati ipo au la.
Isitoshe, tufanye utaratibu wa kuweka nakala kwenye Makumbusho ya Taifa ili kila atakayetaka kuiona katika miaka mingine 50 ijayo na kuzidi aione.
Mwisho, narejea kusema kuwa kwa upande wa Serikali tunasikitishwa na kufadhaishwa sana na tuhuma nzito kwamba labda waasisi wetu hawakuwa makini au walitufanyia kiini macho. Hatukutarajia wawepo Watanzania wenzetu, wafikie hapo.
Ni jambo zito. Vile vile hatukutarajia kuwa Serikali itatuhumiwa kuwa haikuwa makini kuhifadhi waliosaini waasisi wetu.
Matumaini yetu ni kuwa baada ya leo tutaendelea na mambo ya msingi kwa mustakabali, umoja na uimara wa Taifa letu badala ya kuchochea hisia kuwa Muungano wetu hauna msingi imara wa kisheria.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Mapema Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema kuwa Ikulu imemtumia faksi ya hati hiyo na kwamba, amekwishakuikabidhi kwa ofisi ya Mwenyekiti wa Bunge hilo.

Soma hati hii:
The Articles of Union between Tanganyika and Zanzibar

THE ARTICLES OF UNION BETWEEN THE REPUBLIC OF TANGANYIKA AND THE PEOPLES' REPUBLIC OF ZANZIBAR

WHEREAS the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples' Republic of Zanzibar being mindful of the long association of the peoples of these lands and of their ties of kinship and amity, and being desirous of furthering that association and strengthening of these ties and of furthering the unity of African peoples have met and considered the union of the Republic of Tanganyika with the Peoples Republic of Zanzibar:

AND WHEREAS the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples'Republic of Zanzibar are desirous that the two Republics shall be united in one Sovereign Republic in accordance with the Articles hereinafter contained:-

It is therefore AGREED between the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples' Republic of Zanzibar as follows: -

(i) The Republic of Tanganyika and the Peoples' Republic of Zanzibar shall be united in one Sovereign Republic.

(ii) During the period from the commencement of the union until the Constituent Assembly provided for in Article (vii) shall have met and adopted a Constitution for the united Republic (hereinafter referred to as the interim period) the united Republic

(i! ii) to (vi).

shall be governed in accordance with the provisions of Articles

(iii) During the interim period the Constitution of the united Republic shall be the Constitution of Tanganyika so modified as to provide for-

(a) a separate legislature and executive in and for Zanzibar from time to time constituted in accordance with the existing law of Zanzibar and having exclusive authority within Zanzibar for matters other than those reserved to the Parliament and Executive of the united Republic;

(b) the offices of two Vice-Presidents one of whom (being. a person normally resident in Zanzibar) shall be the head of the aforesaid executive in and for Zanzibar and shall be the principal assistant of the President of the United Republic in the discharge of his executive functions in relation to Zanzibar;

(c) the representation of Zanzibar in the Parliament of the United Republic;

(d) such other matters! as may be expedient or desirable to give effect to the united Republic and to these Articles.

(iv) There shall reserved to the Parliament and Executive of the united Republic the following matters-

(a) The Constitution and Government of the united Republic.

(b) External Affairs.

(c) Defence.

(d) Police.

(e) Emergency Powers.

(f) Citizenship.

(g) Immigration.

(h) External Trade and Borrowing.

(i) The Public Service of the united Republic.

(j) Income Tax, Corporation Tax, Customs and Excise.

(k) Harbours, Civil Aviation, Posts and Telegraphs.

And the said Parliament and Executive shall have exclusive authority in such matters throughout and for the purposes of the united Republic and in addition exclusive authority in respect of all other matters in and for Tanganyika.

(v) The existing laws of Tanganyika and of Zanzibar shall remain in force in their respective territories subject-

(a) to any provision made hereafter by a competent legislature;

(b) to such provision as may be made by order of the President of the united Republic for the extension to Zanzibar of any law relating to any of the matters set out in Article (iv), and the revocation of any corresponding law of Zanzibar;

(c) to such amendments as may be expedient or desirable to give effect to the union and to these Articles.

(v) (a) The first President of the united Republic shall be Mwalimu Julius K. Nyerere and he shall carry on the Government of the united Republic in accordance with the provisions of these Articles and with the assistance of the Vice-Presidents aforesaid and of such other ministers and officers as he may appoint from Tanganyika and Zanzibar and their respective public services.

(b) The first Vice-President from Zanzibar to be appointed in accordance with the modifications provided for in Article (iii) shall be Sheikh Abeid Karume.

(vii) The President of the united Republic: in agreement with the Vice-President who is head of the Executive in Zanzibar shall-

(a) Appoint a Commission to make proposals for a Constitution for the united Republic.

(b) Summon a Constituent Assembly composed of Representatives from Tanganyika and from Zanzibar in such numbers as they may determine to meet within one year of the commencement of the union for the purpose of considering the proposals of the Commission aforesaid and to adopt a Constitution for the united Republic.

(viii) These Articles shall be subject to the enactment of laws by the Parliament of Tanganyika and by the Revolutionary Council of the Peoples' Republic of Zanzibar in conjunction with the Cabinet of Ministers thereof, ratifying the same and providing for the Government of the united Republic and of Zanzibar in accordance therewith.

IN WITNESS WHERE Julius K. Nyerere, the President of the Republic of Tanganyika, and Abeid Karume the President of the Peoples' Republic of Zanzibar have signed these Articles, in duplicate, at Zanzibar, on this twenty-second day of April, 1964.

Passed in the National Assembly on the twenty-fifth day of April, 1964.

Source: Mzalendo.net

Msikilize baba wa taifa Mwl. J.K.Nyerere kuhusu ugumu wa maamuzi ya kuunganisha nchi ambao leo hii  ndicho chanzo cha yanayoitwa changamoto za muungano wa smz na smt


0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza