Mwigulu Lameck Nchemba Atangaza Nia Dodoma Leo.


 
Naibu Waziri wa fedha na Mbunge wa Iramba Mwigulu 
Lameck Nchemba ndani ya ukumbi wa Nyerere,
chuo cha Mipango mkoani Dodoma

Leo Jumapili ya tarehe 31/05/2015  Naibu Waziri wa fedha na Mbunge wa Iramba Mwigulu  Lameck Nchemba ndani ya ukumbi wa Nyerere,chuo cha Mipango mkoani Dodoma aweka nia yake ya kutaka kuwa Raisi Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kupitia tiketi ya CCM.


Kauli mbiu ya Mwigulu ni ‘Mabadiliko ni Vitendo Wakati ni Sasa.’
Katika hotuba yake Mwigulu alianza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, wazee, ndugu zake, wananchi wake wa Iramba na wananchi wote waliohudhuria hafla hiyo ya kutangaza nia.

Mwigulu pia amempongeza Rais Kikwete kwa kumuamini na kumteua katika nyadhifa mbalimbali.
Amesema ameamua kutangaza nia akiwa mkoani Dodoma ili kuondoa dhana ya ‘ukwetukwetu’ iliyozoeleka miongoni mwa viongozi wengi.


Akaongeza kuwa Dodoma ni makao makuu ya taifa na chama chake ndiyo maana amefanya hivyo.Na akichaguliwa serikali yake itahamia Dodoma.

Aidha Mwigulu ameeleza mambo matatu yaliyomsukuma kutangaza nia kuwa ni pamoja na:
-Kutaka Mabadiliko
-Kujua mbinu za mabadiliko.
-Utayari wa kufanya mabadiliko.

Kiongozi huyo ameeleza jinsi anavyozijua fika shida za Watanzania na umasikini walionao kwani hajausoma kwenye vitabu bali ameuishi.
Mwigulu ameeleza pia alivyobeba zege baada ya kumaliza chuo kikuu na mke wake akiwa mama ntilie akiwapikia yeye na vibarua wengine wa ujenzi.
Mwigulu awa ni wa tatu ndani ya wana CCM walio jitokeza hadi sasa kutangaza nia.

Leo hii hii  nyakati za saa tano asubuhi hapa jijini Mwanza Mheshiwa Wassira alitangaza nia ya kuwa mmoja wa wanaotarajiwa kuteuliwa na CCM  kugombea Uraisi hapo Octoba ndani ya kumbi maarufu hapa  jijini Mwanza.Kauli mbiu yake ikiwa ni Uadilifu mbele na kusisitizia  siasa za uchumi huria ndani ya falsafa ya Ujamaa kupitia ushirika.

Mwigulu yeye katoka na kauli mbiu ya 'Mabadiliko ni vitendo wakati ni huu.' kama nilivyotangulia kuieleza.

Jana kule Arusha ndani ya viwanja vya Shekh Amri Abeid Mheshimiwa Lowassa alikuja na kauli mbiu ya ; "Elmu kwanza."
Mwigulu toka utotoni mwake wazazi wake wanadhihirisha kuwa ameonesha kuwa na kipaji cha uongozi.Hili limeonekana hadi akiwa shuleni,chuo kikuu mpaka sasa.

Mwigulu anawaomba watanzania na wana CCM kumkubali na akaahidi kuwavusha kufikia uchumi wa kipato cha kati.

Amesema tatizo kuu la nchi  ni rushwa, ubadhirifu na kufanya kazi kwa mazoea. Amewahakikishia watanzaniai kwamba hivyo ndivyo vipau mbele vyake  wakimpa ridhaa ya kuliongoza taifa hili.Kwani anayajua matatizo ya watanzania, amejiandaa na nia anayo.

Aidha aliongezea kwa kusema kuwa yeye amebeba ajenda ya wananchi.na alichokieleza kinatokana na ufahamu wake kwa watanzania na wana CCM. na yuko tayari kuwatumikia kwa moyo wake wote na nguvu zake zote.Akisisitiza kuwa umasikini wa watanzania hakuusoma vitabuni bali ameuishi.

Mwigulu na Familia yake
Shida za maji na madawa anasema ameziishi. Akasimulia kisa cha chumba kilichokuwa kikifumgwa sana wakati wa utoto wao ni chumba cha maji na mtoto aliyekuwa anakunywa maji mara kwa mara alionekana kuwa ni mtoto mkorofi.

Aliendelea kudai kuwa hatakuwa na huruma na uvumilivu  kwa wala rushwa na wahujumu uchumi na atazingatia masilahi ya wafanyakazi.
Kuhusu tatizo la ajira amesema kwa kufufua viwanda ambako vijana watafanya kazi kwa 'shift' kwa hatua hii anaamini itapunguza au kuondoa kabisa tatizo la ajira.

Akisisitizia wajibu wa awamu yake,alieleza mafanikio ya awamu zilizotangulia na mafanikio yaliyopatikana katika awamu hizo.

Alisema awamu ya kwanza  ilifanikiwa katika kutafuta uhuru wa taifa hili  na kujenga misingi ya umoja wa kitaifa na ya pili ilibadili mfumo wa uchumi wa nchi hii na kujenga uwezo  wa watanzania kiuchumi na kupunguza serekali kushikilia njia za kiuchumi kwa asilimia mia moja na kuruhusu kusaidiwa.

Kwa awamu ya tatu akasema  ilijenga taasisi na  mifumo ya huduma za kitaifa. Awamu ya nne imejishughulisha na miundo mbinu, Kujenga rasilimali watu na kujenga misingi ya uchumi wa kisasa.

Akieleza kazi za awamu yake alishauri watu kutompima raisi kwa kile alichofanya kwani hakuna zawadi wanayopewa bali wawapime kwa yale wanayotarajia kufanya.
"Raisi wa awamu ya tano atapimwa kwa kile atakachofanya na si kile alichowahi kufanya."akasisitizia.

Akawabainisha wana CCM na watanzania  wote kuwa yeye  akipewa ridhaa ya kuliongoza taifa hili,afanya mambo makuu matatu, kazi ya kwanza na kubwa kulika zote ni kuipeleka nchi kuwa nchi ya  kipato cha kati na wananchi wake kuwa wananchi wa  kipato cha kati. Kazi ya pili akasema ni kujenga taifa linalojitegemea kibajeti. Kazi ya tatu kuwajenga uwezo wa wananchi wa kumiliki uchumi wao wenyewe.

Akakomelea kwa kusema miaka hamsini ya kuwa taifa ombaoba na la watu masiki hali tunazo rasilimali za kututoa hapo sasa basi ni mwisho.

Kuhusu muungano na ulinzi na usalama wa nchi alisema hivyo vitakuwa pia vipaumbele katika serikali yake.

Kama mpenzi wa michezo,suala la michezo hakuliweka kando. Alimalizia kwa kudai kuwa yako mengi ila kutokana na muda hayo yatatosha kumpima kama anafaa au la.

Aliendelea na suala lake ambalo likuwa kama silaha yake ya mapambano, suala la mazoea."Ukichagua kiongozi kwa mazoea atafanya kazi kwa mazoea na mazoea siku zota ni yale yanayomnufaisha mhusika yeye mwenyewe na si kwa masilahi ya wengi."Mara kadaa alirudia kauli hii.

UKUMBI ULIVYOKUWA UMEJAA.
Taarifa zinadai wako watangaza nia zaidi ya thelathini kutoka kwa CCM peke yake bado hatujaanza kusikia kutoka  vyama vingine. Watanzania kazi kwetu kuwasikiliza na kuchambua upi mpunga kwenye kauli za wanaojinadi hawa na zipi ni pumba.
MWIGULI HAKIKA PAMOJA NA VIJINENO VYA HAPA NA PALE YAELEKEA AKAWA CHAGUO LA WENGI.

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza