Baba Mtu Mzima ( miaka 70) Atuhumiwa Kumwingilia Mbwa (Bestiality )

Mbwwa ni Walinzi na si Wapenzi
Polisi  wa Manisipaa ya mji wa   Moshi Mkoani Kilimanjaro, wanamsaka Bw. Severin Kessy baba mtu mzima mkazi wa kata ya Majengo( miaka 70) kwa tuhuma za kumwingilia mbwa (bestiality ) ndani  ya chumba anakoishi.

Mkuu wa Polisi (RPC) mkoani hapa Kamanda Robert Boaz amesema Bw. Severin Kessy mtuhumiwa mweye wanawake watatu wa ndoa ameshuhudiwa akifanya kitendo hiki na  mbwa  tarehe 3 Aprili mwaka huu.

Bwana Boaz alisema kuwa majirani waliitaarifu Polisi juu ya tukio hili lakini walifika wakiwa wamechelewa na mtuhumiwa akawa ametoroka.

Mkuu huyu wa Polisi akiongea na wana habari alisema mbwa aliyefanyiwa kitendo hiki kisicho cha kawaida ni wa kijana ambaye anaishi nyumba moja na  mtuhumiwa na imedaiwa pia kwamba  majirani wamemshuhudia mtuhumiwa mara kadhaa akimwingilia mbwa huyo siku za nyuma.

Kamanda huyu aliongeza kusema  kwamba pamoja na kumsaka mtuhumiwa Bwana Kessy, wataalamu wa tiba wametakiwa  kumchunguza mbwa huyu ambaye  tokea tukio hili kutokea sehemu zake nyeti zimevimba na anaoneka na hali tofauti na kawaida.

Swali la kujiuliza hapa ni kuwa  hivi hii hali kweli ni ya kawaida au ni masuala ambayo yamegubikwa na ushirikina au ni shetani la ngono.

Mkondo wa sheria unapaswa uchukue nafasi yake na ikibainika kwamba mtuhumiwa ana hatia hatua kali zichukuliwe ili kukomesha matukio ya aibu kama haya.

Isitoshe upimaji wa mtu huyu na wake zake unapaswa ufanyike haraka ili kubaini kama wameadhirika kiafiya au la na kama wameathirika matibabu yafanyike mapema.

Chanzo:Daily News online.

0 comments:

POLL

Which structure of government do you prefer to be implemented in Tanzania?
  
pollcode.com free polls 

TOA MAONI YAKO HAPA (NI BURE)

Name

Email *

Message *

Copyright © 2014 Hii Wiki jijini Mwanza